• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanawake washauriwa kuachana na dhana ya kuwa tegemezi

Imewekwa tarehe: March 6th, 2020

Wanawake nchini wametakiwa kuondokana na dhana ya kuwa tegemezi na wajiingize katika ujasiriamali ili kujikwamua kiuchumi, tukielekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yenye kauli mbiu isemavyo “Kizazi cha usawa kwa maendeleo ya Tanzania ya sasa na ya baadaye”.

Hayo yamesemwa na baadhi ya wanawake Jijini Dodoma, ambapo Husna Juma, binti mjasiriamali alieleza jinsi alivyothubutu na kuanzisha biashara ya kuuza uji na chai na kwamba ndiyo inayomwezesha kuendesha maisha yake.

Husna ambaye ni mama wa watoto wawili anaendesha maisha yake kwa biashara hiyo huku akiwasomesha kutokana na kipato anachokipata katika biashara hiyo.

Alizungumza namna alivyoiona fursa na kuichangamkia alisema “Mimi ni kijana tena mthubutu ambaye niliiona fursa na kuamua kuichangamkia, nilikuwa nauza vocha lakini kuna mama mjamzito alinishawishi, tulikuwa tukifanya kazi jirani kila nikifika ananiuliza kama nimemletea uji” alisema.

Aliendelea kwa kusema kuwa, “Siku ya kwanza nakumbuka nilikuja na chupa moja tu kwa ajili yake lakini cha kushangaza yeye aliambulia kikombe kimoja tu, hapo nikaona fursa nikapata moyo wa kuingia katika biashara hii ambayo wadada wengi hawawezi kutokana na kuidharau”, alisema Juma.

Mbali na fursa hiyo aliyoiona na kuifanyia kazi, pia amekiri uwepo wa changamoto ambazo anakumbana nazo katika biashara yake hiyo hali ambayo mara nyingine inamkatisha tamaa ya kuendelea na kazi hiyo.

“Kazi hii ni ngumu kutokana na mazingira ninayofanyia kazi, wengi wananidharau kwa kile ninachokifanya na kuniona kama napoteza muda, lakini kujiamini kwangu na bidii ndiyo iliyonifikisha hapa.

“Nakumbuka biashara hii nilianza mwaka 2013 nikiwa  na mtaji wa 15,000 lakini hivi sasa nimefikisha mtaji wa laki mbili, hivyo niwashauri tu  wanawake wenzangu tusichague kazi, ilimradi tu ni halali  na inakupatia kipato, ili tuondokane na utegemezi”, alisema mjasiriamali huyo.

Aidha alitoa wito kwa wanawake kuelekea machi 8 mwaka huu ambayo ni siku ya wanawake duniani kuhakikisha wanashiriki ipasavyo katika shughuli zitakazowainua kimaendeleo ili kuweza kuitetea 50-50 ya usawa baina yao na wanaume katika nyanja zote.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.