• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanawake watakiwa kujitathmini katika uongozi

Imewekwa tarehe: March 9th, 2025

Na. Faraja Mbise, DODOMA

Wanawake watakiwa kujitathmini katika nyanja za uongozi kwa kuonesha nia ya kuwajibika ipasavyo na kuchangamkia fursa za uongozi zinazojitokeza katika jamii.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alipokuwa akizungumza na maelfu ya wanawake waliojitokeza katika kongamano la kanda ya kati lililohusisha mikoa mitatu (Dodoma, Singida na Iringa) katika kuelekea kilele cha Siku ya Wanawake Duniani kongamano hilo lilifanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre, Dodoma. 

Senyamule alisema “naomba nitoe shime kila mmoja wetu ajitathmini hatua gani amechukua kuonesha uwezo wake wa kuongoza katika eneo alilopewa. Ni imani yangu kuwa kila mahali tunatosha kwasababu Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameonesha uwezo wa kutosha kwenye nafasi ya urais. Kwahiyo, wanawake tunaweza katika kila eneo”.

Akiongelea kuhusu takwimu za wanawake viongozi wa Mkoa wa Dodoma, alisema karibu ngazi zote za uongozi kuna viongozi wa kike na takwimu zinaonesha uthubutu ni mdogo na hivyo aliwataka wanawake kuongeza uthubutu wa kuwanania nafasi hizo za uongozi.

“Mkuu wa mkoa kwa sababu anatakiwa mmoja, kwahiyo ni asilimia 100 inaongozwa na mwanamke, kwa wakuu wa wilaya ni asilimia 71, kati ya wakuu wa wilaya saba wawili ni wanaume na watano ni wanawake na wanafanya vizuri katika nafasi zao. Tukienda upande wa wabunge, asilimia 11 ni wanawake, katibu tawala tuna asilimia 86, wakurugenzi wa halmashauri asilimia 25 na madiwani asilimia 14 za wanaogombea ni wanawake” alisema Senyamule.

Kwa upande wake, Mfamasia kutoka Hospitali ya Rufaa, Mkoa wa Dodoma, Jackline Moshi, alisema kuwa amejifunza mengi katika kongamano hilo na kuchangamkia fursa zinazojitokeza katika jamii. 

“Tumejifunza mengi sisi kama wanawake, tukayafanyie kazi hasa kujiamini katika nyanja mbalimbali za uongozi, kujiamini katika kufanya kazi, kujiamini katika kila sekta. Tukisimama na wanaume tunaweza” alisema Moshi.

Nae, mkazi wa Dodoma, Rhobi Maro alisema amevutiwa sana na rai iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule na Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anna Makinda ya kuchangamkia fursa katika uongozi. Pia alitoa rai yake kwa wanawake kuendelea kujiamini na kupambana kuchangamkia fursa zinazojitokeza.

“Wameongelea kuchangamkia fursa kujitokeza hasa katika kugombea na kupambana zaidi. Na tunaamini wanawake wengi watajitokeza katika uchaguzi huu wa 2025 kugombea nafasi mabalimbali za uongozi. Natoa rai kwa wanawake wote waendelee kupambana na kujiamini kwamba wanaweza” alisema Maro.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.