• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanufaika wa Mpango wa TASAF washauriwa kujiunga na Bima ya Afya (CHF)

Imewekwa tarehe: September 30th, 2020

WANUFAIKA wa mpango wa kunusuru kaya masikini katika Kata ya Uhuru Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshauriwa kujiunga na mfuko wa afya ya jamii (CHF) iliyoboreshwa kwa shilingi 30,000 ili watu sita waweze kupata huduma ya matibabu bila malipo kwa mwaka mzima.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Nala, Monica Lugaila alipokuwa akiongea na wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini katika Mtaa wa Kipande, uliopo Kata ya Uhuru jijini hapa.

Lugaila alisema kuwa mfuko wa afya ya jamii (CHF) iliyoboreshwa ni muhumu kuwahakikishia uhakika wa matibabu kwa kipindi cha mwaka mzima. Alisema kuwa mtu au watu wanaweza kujiunga na kukata CHF iliyoboreshwa na kupata huduma ya matibabu kwa watu sita kwa mwaka mzima kwa gharama ya shilingi 30,000 tu. Suala la afya ni muhimu kwa kila mtu, maandalizi ya mapema kabla ya kuugua ni muhimu ili kuepuka kutumia gharama kubwa pindi anapougua, aliongeza.

Aidha, Afisa huyo alisema kuwa zoezi hilo la uhawilishaji fedha linafanyika kwa wanufaika waliohakikiwa katika kipindi cha uhakiki tarehe 30 Julai, 2020 ndiyo wanaohusika na zoezi hilo. “Katika zoezi hili, hakuna utaratibu wa kuchukuliana fedha, kila mnufaita alitakiwa kuchukua fedha yake mwenyewe. Kwa wale wanufaika ambao hawakuweza kufika kutokana na sababu mbalimbali kama ugonjwa, tuliwafuata nyumbani na kila mmoja alilipwa malipo anayostahili na kusaini kwa mujibu wa taratibu” alisisitiza Lugaila.

Akiongelea utekelezaji wa zoezi la uhawilishaji fedha, mratibu wa tasaf Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sekunda Kasese alisema kuwa zoezi hilo limepangwa vizuri. “Kwa siku ya leo, zoezi la uhawilishaji fedha litafanyika katika mitaa 28, iliyopo katika kata 13 za Jiji la Dodoma. Katika mitaa hiyo, jumla ya wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini 1,645 wanatarajia kupokea malipo ya shilingi 104,828,000. Nikumbushe tu kuwa zoezi hili litahusha madirisha mawili ya malipo yaani awamu mbili zitalipwa kwa pamoja” alisema Kasese.

Kwa upande wake mlengwa wa mpango wa TASAF, Tatu Ndala, alisema kuwa zoezi hilo la uhawilishaji fedha lilifanyikavizuri na kwa uwazi. “Watu wa TASAF walipofika kwanza walitupa mafunzo na kutuhamasisha kuhusu CHF iliyoboreshwa na watu wasiokuwa na namba za NIDA waliorodheshwa majina yao ili kuwasaidia kupata namba hizo. NAona safari hii walikuwa wamejipanga vizuri sababu hapakuwa na msongamano wa wat una mambo yalienda haraka haraka. Mimi namshukuru sana Mungu kwa sababu TASAF imenisadia sana kuanzisha shughuli ya Mama lishe ambayo inaniwezesha kuishi kwa uhakika” alisema Ndala.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.