• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wasimamizi miradi Jiji la Dodoma watakiwa kuwa wazalendo

Imewekwa tarehe: December 14th, 2024

Na. Faraja Mbise, DODOMA

WASIMAMIZI wa miradi ya ujenzi katika Shule ya Sekondari Matumbulu wametakiwa kuwa wazalendo na kutokwamisha juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, alipokuwa akikagua miradi ya ujenzi wa Shule ya Sekondari Matumbulu iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

“Matamanio ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuleta hizi shule ni kwasababu watoto wasitembee umbali mrefu. Bado sisi Mkoa wa Dodoma tuna utoro na baadhi ya changamoto inayochangia utoro ni watoto kutembea mwendo mrefu kwenda shule. Kwahiyo, anaona fahari asiende shuleni. Lakini tuna ukatili wa kijinsia, kati ya maeneo ambayo watoto wanafanyiwa ukatili ni akiwa anaenda shuleni, wanapita maporini kwasababu ya umbali mrefu, yote haya Rais ametaka ayamalize kwa kuwajengea shule karibu na eneo lao” alisema Senyamule.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi, alitoa rai kwa wafanyakazi kuweka mbele uzalendo ili kuhakikisha miradi hiyo inasonga mbele kwa wakati na kwa viwango vya juu.  “Ni rai kwa wenzangu na mimi mwenyewe, tuweke mbele uzalendo ili tuweze kuhakikisha miradi hii inakamilika kwa wakati, kwa viwango vilivyokusudiwa na kuzingatia thamani ya fedha ili tuweze kufikia lengo lililokuwa limekusudiwa” alitoa rai Mbugi.

Mradi huo wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Matumbulu unatarajiwa kukamilika ifikapo Desemba 31, Mwaka huu. Shule hiyo ilitengewa jumla ya Shilingi Milioni Mia tano arobaini na nne, laki mbili, ishirini na tano elfu na mia tano ishirini na sita (544,225,526) kwa ujenzi wa miundombinu ya shule ikiwa ni pamoja na madarasa nane na ofisi mbili yanayogharimu shilingi 192,628,542, Jengo la Utawala shilingi 71,491,667, Maabara ya Fizikia 50,000,000 Maabara ya Baiolojia na Kemia 100,000,000, Jengo la Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) 56,969,143, Choo shilingi 18,700,000, Kichomea taka 3,833,333 na Tanki la maji 3,641,667.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.