• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wasimamizi vituo vya kupigia kura watakiwa kufanya kazi kwa weledi

Imewekwa tarehe: November 25th, 2024

Na. Dennis Gondwe, MTUMBA

WASIMAMIZI wa vituo vya kupigia kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 wametakiwa kufanya kazi kwa weledi na uzalendo wakizingatia kanuni na taratibu ili kuweza kufanikisha uchaguzi huo.

Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akifungua mafunzo kwa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura, tukio lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba.

Dkt. Sagamiko alisema kuwa wasimamizi hao wapo kwa ajili ya kuapishwa na kupewa mafunzo kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kutokana na sifa na uwezo wao katika utendaji kazi ndiyo zimewafanya waweze kuchaguliwa. “Tunahitaji kuongeza umakini na usikivu wakati huu wa mafunzo. Hata kama ulisimamia uchaguzi uliopita, huu ni wa mwaka 2024 na haujawahi kufanyika popote. Hivyo, kuna utofauti kati ya uchaguzi huu na uchaguzi uliopita. Moja ya mabadiliko ni mabadiliko ya kanuni, niwasihi muongeze umakini katika kusikiliza ili tusiende kuharibu uchaguzi huo. Miongoni mwa mambo ambayo hutakiwi kucheza nayo ni uchaguzi. Uchaguzi unatoa hatima ya usalama na utulivu wa taifa letu. Maendeleo yanategemea hali ya usalama katika Jiji letu. Hivyo, tekelezeni jukumu hili kwa kuzingatia uzalendo” alisema Dkt. Sagamiko.

Wakati akiwakaribisha alisema “karibuni kwenye ukumbi maridhawa na bora kabisa wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma hapa Mji wa Serikali Mtumba. Niwapongeze kwa kupata nafasi kuteuliwa kuwa wasimamizi wa vituo kwa uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Jiji lina watumishi zaidi ya 5,000 na mliobahatika ni kama 1,050. Ni kutokana na weledi wenu, sifa zenu na uzalendo wenu kwa taifa letu. Leo mtaapishwa, mkaishi kiapo ili kiwe dira na makatazo ya mambo ambayo hamtakiwi kufanya wakati wa uchaguzi” alisema Dkt. Sagamiko.

Nae Mwakilishi wa Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) Mkoa wa Dodoma, Zacharia Mwandumbya aliwataka wasimamizi wa vituo vya kupigia kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 kutojihusisha na vitendo vya rushwa katika uchaguzi huo. “Ni vema mtakapoapishwa mkafanye kazi kwa uadilifu kama mlivyoelekezwa na viongozi wenu” alisema Mwandumbya.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.