• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura Waaswa kuviishi viapo vyao

Imewekwa tarehe: November 24th, 2024

Na. Faraja Mbise, DODOMA

Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameaswa kuviishi viapo vyao walivyoapa ili wawe na muongozo mzuri pindi watakapokuwa katika vituo vyao vya kazi ifikapo tarehe 27 Novemba, 2024.

Hayo yalisemwa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akifungua semina ya wasimamizi wa vituo vya kupigia kura iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba.

“Mtaenda kuapishwa, naomba mkaishi kiapo mtakachokipata, ili iwe dira na ndio yawe makatazo ya mambo ya kutokufanya wakati wa usimamizi” alisisitiza Dkt. Sagamiko.

Akiongelea kuhusu kanuni na taratibu za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, aliwasisitiza wasimamizi wa vituo vya kupigia kura, kufuata kanuni za uchaguzi za mwaka huu 2024, kwasababu ni tofauti na kanuni za uchaguzi uliopita. Hivyo, aliwataka kuwa makini ili wasifanye makosa ifikapo tarehe 27 Novemba, 2024. “Najua wapo waliowahi kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019, Naomba niwaambie tunahitaji kuongeza umakini na usikivu wakati huu wa mafunzo, hata kama ulikuwa umesimamia mwaka 2019, uchaguzi huu ni wa mwaka 2024 na haujawahi kufanyika popote, utafanyika tarehe 27 Novemba, 2024. Na kama ni wafuatiliaji yapo mengi ya tofauti kati ya chaguzi za Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu. Moja ya tofauti ni mabadiliko ya kanuni. Kanuni zilizotumika katika uchaguzi wa 2019 na chaguzi nyingine kabla ya hapo ni tofauti sana na kanuni zinazotumika mwaka huu. Hivyo, niwasihi muongeze umakini katika kusikiliza ili tusiende kuharibu siku hiyo. Bahati nzuri wengi wenu ni walimu na miongoni mwenu mlishawahi kusimamia kazi maalumu na sisi tunasema miongoni mwa mambo ambayo hautakiwi kucheza nayo mojawapo ni uchaguzi, nafikiri ni miongoni mwa yale mambo makuu ambapo ukipata nafasi ya kushiriki unakosa usingizi ni pamoja na uchaguzi. Uchaguzi unatoa hatima ya usalama na utulivu wa taifa letu. Maendeleo ya sehemu yoyote yanategemea sana hali ya usalama katika eneo husika” alisema Dkt. Sagamiko.

Akiongelea kuhusu sifa na vigezo vilivyotumika kuchagua wasimamizi wa vituo vya kupigia kura, alikanusha madai ya kuwa wasimamizi hao walichaguliwa kwa upendeleo. “Leo mtapata mafunzo mafupi lakini pia zoezi kubwa la kuapishwa, kuwa rasmi kwenda kusimamia vituo vyetu kwa siku ya uchaguzi. Ninajua wapo wenzenu ambao waliwauliza kwanini mimi nimekosa na wewe umepataje? wengi wanaweza wakahisi kwamba kuna watu juu yenu waliofanya muwe hapo lakini niwahakikishie ni sifa zenu ndizo zilizowafanya muwe hapo” alisisitiza Dkt. Sagamiko.

Aidha, aliwapongeza wasimamizi wa vituo vya kupigia kura kwa kuchaguliwa kuwa miongoni mwa wasimamizi wa vituo siku ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. “Niwapongeze sana kwa kupata nafasi ya kuteuliwa kuwa miongoni mwa wasimamizi wa vituo siku ya tarehe 27 Novemba, 2024 kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Jiji la Dodoma lina watumishi takribani 5,000 tano ‘plus’ na mliobahatika takribani 1,450 na, mnaweza mkaona ni namna gani mchujo ulikuwa mgumu, lakini niwaambie tu ni kutokana na weledi wenu, sifa zenu na uzalendo wenu kwa taifa letu, ndio maana leo mpo hapa kwa ajili ya kupata mafunzo mafupi lakini kwa tukio kubwa kabisa la kuapishwa” alipongeza Dkt. Sagamiko.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.