• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Watanzania, sasa madini yao yameanza kuwanufaisha - Rais Magufuli

Imewekwa tarehe: October 13th, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli leo tarehe 13 Oktoba, 2020 ameshuhudia kampuni ya Twiga Minerals na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) likitoa gawio kwa Serikali kutokana na faida katika biashara ya madini.

Halfa ya utoaji wa gawio hili imefanyika katika ukumbi wa kituo cha kimataifa cha mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam ambapo kampuni ya Twiga Minerals imekabidhi Dola za Marekani Milioni 40 (sawa na takribani shilingi Bilioni 100 za kitanzania) na STAMICO imekabidhi shilingi Bilini 1.1 kwa Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango.

Aidha, katika hafla hiyo wachimbaji wadogo wa madini kupitia chama chao (FEMATA) wametoa tuzo kwa Mhe. Rais Magufuli kwa kutambua mchango wake mkubwa wa kulinda maslahi ya wachimbaji wadogo na maslahi ya Watanzania katika rasilimali yao ya madini.

Waziri wa Madini, Mhe. Dotto Biteko amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa dhamira yake ya dhati na mwongozo wake katika usimamizi wa madini ambao umesaidia kubadili sekta ya madini kutoka sekta iliyofichwa na isiyo na maslahi kwa Watanzania na kutwa sekta inayofanyika kwa uwazi na inayowanufaisha Watanzania kwa kuchangia fedha nyingi katika pato la Taifa, kutoa ajira na kustawisha jamii.

Mhe. Waziri Biteko ametoa mfano kuwa kati ya mwaka 2015/16 na mwaka 2019/20 mapato ya madini yameongozeka kutoka shilingi Bilioni 168 hadi shilingi Bilioni 528 na kwa sehemu kubwa shughuli za madini zinafanywa na Watanzania wanyewe badala ya kufanywa na wageni kama ilivyokuwa zamani.

Katika hotuba yake, Mhe. Rais Magufuli ameelezea kufurahishwa kwake na mafanikio makubwa ambayo Tanzania imeyapata baada ya kuchukua hatua za kutunga sheria mpya ya madini kudhibiti wizi na utoroshaji wa madini na kunzisha masoko ya madini na ameewakata Watanzania wote kutembea kifua mbele kwa kuwa sasa madini yao yameanza kuwanufaisha.

Mhe. Rais Magufuli amesema Tanzania imejaliwa kuwa na utajifiri wa aina mbalimbali za madini kama gesi na mafuta hivyo ni wakati wa Watanzania kuamka na kuchamgamkia fursa za uchimbaji na uwekezaji katika rasilimali hizo bila kujali hadhi ya mtu, kampuni ama taasisi, ilimradi hawavunji sheria na wanalinda maslahi ya Taifa kwa kulipa kodi na tozo mbali mbali za kisheria.

Amewashangaa Watanzania ambao walikuwa wakipinga hatua zilizochukuliwa na Serikali kurekebisha dosari zote zilizosababisha Watanzania kutonufaika na madini yao ikiwemo kukamata makinikia ya dhahavu, kudhibiti wizi na utoroshaji, kupitia upya mikataba ya madini, kudai fidia na kutunga sheria zilizoiwezesha nchi kuwa na umiliki wa asilimia 16 katika migodi ya madini na kupata mgao wa 50/50 katika faida ya biashara ya madini.

Mhe. Rais Magufuli ameipongeza kampuni ya Barrick Gold ambayo ilikubali kuingia katika majadiliano na Serikali na matokeo yake kuundwa kwa kampuni ya Twiga Minerals ambayo leo imekabidhi gawio la shilingi Bilioni 100, na pia ameipongeza kamati iliyoongozwa na Prof. Palamagamba Kabudi ambayo iliiwakilisha Serikali katika majadiliano hayo, kwa kutekeleza jukumu hilo kwa uzalendo mkubwa licha ya kuzingirwa na vishawishi vya rushwa na hatari za kiusalama.

Aidha, Mhe. Rais Mafgufuli amesisitiza kuwa Tanzania ni mahali salama pa uwekezaji na ametoa wito kwa wafanyabiashara na wawekezaji mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kuja kuwekeza hapa nchini katika sekta mbalimbal ikiwemo madini, na kwamba Serikali itakuwa tayari wakati wote kutoa ushirikiano utakaofanikisha uwekezaji huo ilimradi kuwepo mazingira ya  mwekezaji kupata na Serikali kupata (win-win).

Mhe. Rais Magufuli amewashukuru viongozi wa Dini na Watanzania wote kwa maombi na dua kwa Taifa na amewataka kuendelea kufanya hivyo kwa kuwa Taifa linalosimama na Mungu hufanikiwa, kama ambavyo Tanzania imefanikiwa katika maeneo mengi ikiwemo kuepusha ugonjwa wa Corona (Covid-19) na kusimama kidete kutetea maslahi ya Watanzania.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.