• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Watanzania tuendeleze misitu kukabiliana na athali za mabadiliko ya tabianchi - Dkt. Ndumbalo

Imewekwa tarehe: February 10th, 2022

Waziri Dkt. Ndumbaro awaasa wananchi wafanye matumizi endelevu ya misitu badala ya kukata miti ovyo hali inayoweza kusababisha mabadiliko ya tabianchi.

Dkt. Ndumbaro ametoa rai hiyo jana wakati akizungumza na wadau mbalimbali mara baada ya kushiriki zoezi la upandaji miti katika eneo la Iyumbu jijini Dodoma.

Alibainishata kuwa asilimia 54 ya eneo la nchi yetu ambayo ni sawa na hekta 400 ni misitu, hivyo kila mwananchi analo jukumu la kuitunza na kuendelea kupanda miti mingine ili Tanzania iendelee kuwa ya kijani na kuleta faida.

“Ndugu zangu faida za misitu tunazijua, misitu ni mali kwa sababu watu wanaoishi Mafinga mkoani Iringa na maeneo mengine misitu ndio biashara yao na hata kule nchini Norway misitu inachangia sana kwenye GDP (pato la taifa),” alisema.

Aidha, Waziri Dkt. Ndumbaro aliongeza kuwa kutokana na umuhimu wa misitu hiyo asilimia 3.5 ya Pato la Taifa inachangiwa na sekta hiyo hapa nchini hivyo alisisitiza umuhimu wa kuilinda.

Hivyo, aliipongeza Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kuratibu Wiki ya Mazingira kuelekea kilele cha uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021 na kushiriki zoezi la upandaji miti kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), katika msimu huu wa mvua waliotoa miche ya miti mbalimbali ambayo imepandwa leo katika eneo la Greenpark, Iyumbu jijini Dodoma.

Alisema miti hiyo itasaidia kukabiliana na madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabianchi ambayo yameendelea kushuhudiwa kutokana na mabadiliko yake kuja na athari hasi nyingi zikiwemo kuongezeka kwa joto duniani, kuongezeka kwa baridi, pamoja na kubadilika kwa misimu ya hali ya hewa.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga alitoa wito kwa wananchi kupanda miti katika maeneo yao ili kuendelea kuifanya nchi kuwa ya kijani na mfano wa kuigwa.

Bi. Maganga alisema zoezi la upandaji ni kielelezo cha kutoa hamasa na kuhamasisha maeneo mengine nchi nzima kupata uelewa kuhusu dhana nzima ya kuifanya nchi nzima kuwa ya kijani na ya mfano kupitia kampeni ya Kijanisha Dodoma.

Pia aliwashukuru wadau mbalimbali wa mazingira waliojitokeza katika zoezi hilo, hatua itakayoleta hamasa kwa wananchi ili waweze kufanya shughuli za upandaji miti na kuhifadhi mazingira kuwa sehemu ya maisha yao.

Nae Kamishna wa Uhifadhi kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos. Santos Silayo alisema nchi yetu imejaliwa kuwa na misitu ya aina mbalimbali ikiwemo ya kupanda na kuota kwa asili.

Prof. Silayo aliwataka wananchi kuwa na utamaduni wa kuitunza misitu iliyopo kwani ina mchango mkubwa katika sekta ya viwanda ambayo imekuwa kwa kasi kubwa hapa nchini.

Aliongeza kusema kuwa katika miaka mitatu iliyopita tulishuhudia viwanda takriban 800 vikiwemo vya kati na vikubwa vikianzishwa sambamba na ukuaji wa teknolojia huku akitolea mfano wa nguzo za umeme zinazozalishwa hapa nchini kutokana na misitu.

Kamishna huyo alisema Ukuaji wa viwanda umekwenda kwa kasi kubwa na hata tunashuhudia viwanda vya mkaa mbadala ambavyo vyote vinaleta mchango mkubwa katika kuhifadhi mazingira.

Chanzo: Tovuti Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira)

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.