• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Watanzania tuwe wamoja na kuzingatia maadili - Dkt. Mpango

Imewekwa tarehe: June 12th, 2021

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amefungua mkutano mkuu wa nne wa Mtandao wa Sala na Maombi ya Kitaifa na Kimataifa katika Ukumbi wa Morena Jijini Dodoma huku akiwataka watanzania kuendelea kuwa wamoja kwa kuzingatia maadili,uadilifu na misingi ya utawala bora.

Dkt. Mpango ameyasema hayo jana Jijini hapa wakati wa mkutano huo ulioandaliwa na Taasisi ya Kingdom Leadership Network Tanzania,uliotanguliwa na maombi ya kuliombea Taifa na Viongozi kwa ujumla kwa lengo la kuiongoza nchi kwa misingi ya kufuata utawala bora na uadilifu .

Mkutano huo wa  kitaifa   umeshirikisha viongozi mbalimbali wa kiserikali ndani na nje ya nchi pamoja na Viongozi wa Dini.

Akiongea katika Mkutano huo alisema Serikali ya awamu ya sita ya Rais Samia Suluhu Hassan itaendelea kufuata misingi ya utawala bora na utawala wa Sheria.

Alisema kuwa wao kama Serikali watahakikisha wanafuata misingi ya utawala bora kwa kuzingatia uwajibikaji,uwazi na uadilifu kwa lengo la kuleta haki kwa watu wanaowaongoza.

Katika hatua nyingine amesema kuwa katika kuelekea uchumi wa viwanda, Serikali itajikita katika ushindani wa kibiashara pamoja na kuondoa vikwazo kwa wawekezaji huku akitumia fursa hiyo kuwa wakaribisha wawekezaji wa nje ya nchi kuja kuwekeza nchini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Kingdom Leadership Network Tanzania, (KLNT)ambao ndiyo waandaji wa Mkutano huo Fredrick Ringo alisema dhumuni la mkutano ni kuombea nchi kila mwaka kwa kushirikisha viongozi mbalimbali wa serikali, wabunge na Wafanyabiashara.

Alisema, kwa kuliombea Taifa, Mwenyezi Mungu huepusha dhoruba na kuifanya nchi kuendelea kuwa na utulivu hali itakayowezesha wananchi wake kuwa huru katika kujijenga kiuchumi.

"Kupitia Mkutano huu,tunamwomba Muumba wetu aisaidie Tanzania hasa viongozi waliopo madarakani waweze kutenda  haki kwa   kufuata misingi ya utawala bora katika kuongoza wananchi,"alisema.

Naye Dkt. Charles Sokile ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Biashara cha Joseph na ni Mkurugenzi wa mahusiano ya kimataifa wa Taasisi hiyo alisema kupitia mkutano huo wamepata fursa ya kutangaza rasmi uhusianao wa kibiashara na marekani.

Alisema hali hiyo itasaidia kuunganisha biashara za Tanzania na marekani katika maeneo makubwa sita ikiwemo utalii pamoja na kutangaza mpango rasmi wakuanzisha kituo kidogo cha biashara.

"Hii itasaidia biashara zisizo rasmi ziwe rasmi kwa maendeleo ya uchumi wa Taifa," alisisitiza.

Kutokana na hayo naye Sophia Mwakagenda Mbunge wa Viti maalum,alieleza umuhimu wa kuwa na uwazi na uwajibikaji kwa viongozi hasa katika  kumtanguliza mungu kwa maombi.

Alisema, pamoja na changamoto Dunia inazozipitia lazima watu wasimame pamoja kwa kipindi chote bila kujali itikadi za kidini au siasa.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.