• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Watendaji Kata wahimizwa kuwahi kazini na kupinga vitendo vya rushwa

Imewekwa tarehe: September 13th, 2019

KAIMU Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Balthazar Ngowi amewataka watendaji wa Kata kuwa mfano kwa kuwahi kazini na kupinga vitendo vya rushwa katika maeneo yao ya kazi ili kuwezesha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Kauli hiyo aliitoa hivi karibuni alipokuwa akifungua mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo maafisa watendaji wa Kata ili waweze kusimamia afua za Lishe katika Kata zao tukio lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Ngowi alisema kuwa watendaji wa Kata wanatakiwa kuwahi kazini na kutoa huduma bora kwa wananchi. “Nasema hili, siyo kwamba watendaji wote mnachelewa, hapana. Lakini nalisisitiza kwa sababu wapo watendaji wachache wanaochelewa na kuchelewa kwao kunasababisha ucheleweshaji wa kutoa huduma” alisema Ngowi. Aidha, aliwataka watendaji hao kusimamia na kuhamasisha ulipaji kodi ya serikali katika Kata. Serikali inaendeshwa kutokana na kodi, ambayo inapokusanywa vizuri inapelekwa katika kuboresha utoaji wa huduma za jamii, aliongeza.

Ngowi, ambaye pia ni mkuu wa idara ya Utumishi na Utawala katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma aliwataka watendaji hao kujiepusha na vitendo vya rushwa.  “Mnajua nyie maafisa watendaji ni watawala katika maeneo yenu. Na sifa ya mtawala ni kutokuwa na viashiria vya rushwa. Mnatakiwa kusimamia haki katika utendaji wenu wa kazi ili wananchi wapate huduma bora” alisisitiza Ngowi.

Akiongelea tatizo la lishe kwa watoto katika Kata, alisema kuwa watendaji ni sehemu ya kuchochea tatizo hilo. Aidha, aliwataka kuhamasisha na kusimamia masuala ya lishe vizuri katika Kata zao.

Kwa upande wake Afisa Lishe wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Semeni Eva Juma alisema kuwa hali mbaya ya utapiamlo inasababishwa na ulishaji duni, maradhi ya mara kwa mara na huduma hafifu za malezi na makuzi ya awali ya watoto wadogo. “Utapiamlo unachangia maradhi, vifo na uchelewaji wa ukuaji wa mwili na maendeleo ya akili kwa watoto” alisema Juma.

Akiongelea malengo ya mkataba baina ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji na watendaji wa Kata, alisema kuwa lengo kubwa ni kufanikisha suala la kuboresha hali ya lishe na kupunguza athari za utapiamlo katika jamii. Malengo mengine aliyataja kuwa ni kuhakikisha jamii kupitia uongozi wa Kata inashiriki ipasavyo katika kupanga, kutekeleza na kufuatilia maendeleo ya utekelezaji wa mpango wa Halmashauri na afua za lishe.

Akiongelea mafunzo hayo, afisa mtendaji Kata ya Hombolo Makulu, Aletas Bakindikile alisema kuwa uelimishaji ulikuwa mzuri. “Kwa upande wangu ni mambo yanayoelezeka kila siku katika jamii, hivyo sijaona jambo geni bali kutukumbushia tuendelee kutoa elimu ya lishe ili jamii nzima na vizazi vyetu viendelee kunufaika kupitia elimu ya lishe” alisema Bakindikile.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.