• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Watoa huduma za Afya 3000 kupewa mafunzo ya kuzuia Magonjwa yasiyoambukiza

Imewekwa tarehe: October 24th, 2022

MKURUGENZI wa huduma za tiba Wizara ya Afya Prof. Paschal Ruggajo amesema, jumla ya Watoa huduma za Afya 3000 wa mikoa 26 kupewa mafunzo ya utoaji huduma za kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza ili kuwakinga wananchi ifikapo Desemba 2023.

Prof. Ruggajo amesema hayo leo Oktoba 24, 2022 Jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo ya kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza kwa Watoa huduma za Afya, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali katika mapambano dhidi ya magonjwa hayo.

"Moja kati ya mikakati iliyopo ni kuimarisha huduma za msingi kuwapa mafunzo Watoa huduma za Afya juu ya utoaji wa huduma za kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza. Watoa huduma 3000 kufikiwa kutoka Mikoa 26", Amesema Ruggajo

Amesema, moja kati ya mikakati iliyopo ni kuimarisha huduma za msingi kwa kuvijengea uwezo vituo vya Afya 600 kwa kuwapa mafunzo Watoa huduma za Afya juu ya utoaji wa huduma za kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza utaosaidia katika kuwahudumia wananchi.

Sambamba na hilo, Prof. Ruggajo amesema, Mafunzo haya yanayofanyika sasa ni awamu ya IV, hadi kufikia 28 Oktoba 2022, jumla ya watoa huduma 400 kutoka katika vituo vya Afya 94 vya mikoa minne ambayo ni Dodoma, Lindi,Songwe na Kigoma watajengewa uwezo katika kutoa huduma za magonjwa yasioambukiza.

Aidha, Prof. Ruggajo amesema, mafunzo haya kwa Watoa huduma yatakuwa msaada mkubwa kwa jamii kwani watatumika katika kutoa elimu ikiwemo kuishi mtindo wa Maisha unaofaa kama kuacha tabia bwete na kufanya mazoezi, kuzingatia ulaji unaofaa, kuepuka matumizi ya pombe yaliyopita kiasi na kuepuka matumizi ya tumbaku.

Naye, Mkurugenzi Msaidizi magonjwa yasiyoambukiza Dkt. James Kihologwe amesema, utafiti uliofanyika 2020 wa kuangalia utayari wa kutoa huduma ulionesha vituo vya kutolea afya nchini vipo tayari kutoa huduma za magonjwa yasioambukiza kwa chini ya asilimia 50%, tofauti na huduma nyingine kama huduma ya mama na mtoto na huduma za UKIMWI ambazo zilikuwa zikotolewa kwa takribani asilimia 94.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.