• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Watoto kulindwa dhidi ya ukatili wa kijinsia wilayani Dodoma

Imewekwa tarehe: December 15th, 2024

Na. Asteria Frank, DODOMA

Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Rachel Balisidya amewataka wazazi kuwalinda watoto wao dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia na kuhakikisha wanaweza kutimiza ndoto na malengo yao kwa kuzuia madhara yanayoweza kuwaharibia maisha kisaikolojia.

Wito huo aliutoa leo alipomuwakilisha Katibu Tawala wa Wilaya ya Dodoma kwenye Tamasha la Tanzania Shiriki Malezi Endelevu Kupinga Ukatili (TASHMEKU) katika Shule ya Sekondari Dodoma Makulu kwa lengo la kupinga ukatili wa kijinsia kwa watoto.

Balisidya alisema kuwa Wilaya ya Dodoma bila ukatili inawezekana. Alisema kuwa ipo changamoto ya ukatili kwa watoto na asilimia kubwa ya ukatili inaanzia nyumbani kupitia baba, mama, mjomba, mwalimu na wale wanaowazunguka na kuwaharibu watoto kisaikolojia kwa kuwatesa, kubakwa na kuwanyima haki zao za msingi. “Tuhakikishe katika kipindi hiki cha likizo tuendelee kutoa elimu kwa wazazi ili kulinda usalama wa watoto na kuwalinda na wale watu wanaofanya ukatili juu yao. Wazazi wanatakiwa kuhakikisha wanakuwa karibu na watoto wao ili kuwalinda na waweze kuwaambia ukweli kuhusu jamii ilivyo kwa sasa” alisema Balisidya.

Kaimu Afisa Mtendaji wa Kata ya Dodoma Makulu, Method Karoly aliwaomba wazazi kupinga ndoa za utotoni kwa sababu wanawaumiza watoto wanaozaliwa kwa kutopata malezi mazuri kutokana na wazazi wenyewe kuwa wadogo na wapo chini ya umri wa miaka 18 na kukosa malezi bora. Alisema kuwa ndoa za utotoni pia ni ukatili wa kijinsia na kuliko waolewe ni bora watoto wapewe elimu ili iweze kujisaidia wao wenyewe. “Watoto wanaoingia kwenye ndoa za utotoni wanakutana na mambo mengi sana ya ajabu na hivyo, akili zao zinaharibika mpaka wanakuwa wanashindwa hata kuwalea watoto wao na wanachukulia ndoa za utotoni ni za kawaida na kuwafanyia hivyo kizazi chao pia”. alisema Karoly.

Nae, Wanafunzi wa Shahada ya Sheria Mwaka wa Pili Chuo Kikuu cha Dodoma, Jamal Mwasanjala alisema madhara wanayopata watoto wanaofanyiwa ukatili ni pamoja na kupata tatizo la afya ya akili, huzuni na kushidwa kuongea mambo ya msingi akiwa na watu. “Asilimia kubwa watoto wengi wanakuwa na tatizo la afya ya akili kwasababu malezi waliyopewa ni malezi magumu unaweza kushangaa mtoto anakaa na mzazi wake lakini anashindwa kuongea hata na mzazi kuhusu tatizo au madhara na chanzo cha unyanyasaji mtoto aliopitia” alisema Mwasanjala.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.