• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Watumishi wa umma Dodoma wahimizwa kushiriki zoezi la usafi wa mazingira

Imewekwa tarehe: June 15th, 2019

WATUMISHI wa umma katika Halmashauri ya jiji la Dodoma wameshauriwa kushiriki kikamilifu katika zoezi la usafi wa mazingira katika maeneo yao na maeneo yanayopangwa na serikali kufanyiwa usafi ili wawe mfano bora kwa jamii.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Idara ya Usafi wa Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alipokuwa akiongea na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa zoezi la usafi wa mazingira lililoambatana na maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma na kufanyika katika Kata ya Viwandani Jijini Dodoma leo.

Kimaro alisema kuwa zoezi la usafi wa mazingira ni zoezi la wananchi wote, watumishi wa umma wakiwemo, hivyo wanatakiwa kushiriki kikamilifu. Watumishi wa umma ni kielelezo katika jamii inayowazunguka katika kusimamia na kutekeleza maelekezo ya serikali, aliongeza. Aidha, alisema kuwa watumishi hao kujitokeza kushiriki katika usafi wa mazingira ni njia ya kujiweka karibu na wananchi na taasisi wanazofanyia kazi kufahamika vizuri kwa wananchi.

Akiongelea tathmini ya zoezi la usafi wa mazingira katika Kata ya Viwandani eneo la Chako ni chako na maeneo ya jirani, Kimaro alisema kuwa wananchi wamejitokeza kwa wingi kufanya usafi katika mitaro na maeneo ya wazi. “Changamoto kubwa katika Kata ya Viwandani eneo maarufu la Chako ni chako, wafanyabiashara wanapofanya biashara usiku hawafanyi usafi katika maeneo yao na asubuhi hawaji kufanya usafi na kusababisha kero kwa watumiaji wa maeneo hayo na mazingira kwa ujumla. Mitaro tumekuta ni michafu na wahusika wanaenda kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ndogo za halmashauri ya jiji” alisema Kimaro.

Kwa upande wake, Afisa utumishi katika Halmashauri ya jiji la Dodoma, Joyce Kisege aliyeshiriki zoezi hilo alisema kuwa watumishi wa umma wanawajibu wa kipekee kushiriki katika usafi wa mazingira. “Watumishi wa umma ni sehemu ya jamii hivyo huwezi kuwatenganisha na jamii inayowazunguka. Kwa kushiriki kwao katika masuala ya usafi wa mazingira kuna halalisha usehemu yao katika jamii na kuwaweka karibu na wananchi. Hivyo, huduma wanazotoa zinaweza kuanzia hukohuko katika jamii kabla ya kufika ofisini” alisema Kisege. Aidha, aliongeza kuwa watumishi hao ni sehemu ya uhamasishaji jamii kwa ujumla. Wananchi wanapoona watumishi wa umma wanashiri katika zoezi la usafi wanahamasika kufanya usafi, aliongeza Kisege.

Mkazi wa kaya ya viwandani, juma Abdallah alisema kuwa ushiriki wa watumishi wa umma unaondoa tofauti kati ya watumishi hao na jamii inayowazunguka.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma inatekeleza zoezi la usafi kitaifa kila wiki ya mwisho wa mwezi na kufuatia agizo la mkuu wa mkoa wa Dodoma kuwa zoezi la usafi wa mazingira lifanyike kila siku ya jumamosi limekuwa likitekelezwa.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.