• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Watumishi watakiwa kujilinda na uhalifu wa Mtandao

Imewekwa tarehe: October 19th, 2022

Watumishi wa umma na binafsi wametakiwa kuwa makini na chochote wanachofanya mtandaoni ili kujilinda na changamoto za uhalifu wa mtandao ambapo katika zama hizi za kidijiti taarifa binafsi au za taasisi zimegeuka kuwa malighafi muhimu kwa wahalifu wa mtandao.

Hayo yamezungumzwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Usalama Mtandao wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Stephen Wangwe wakati akitoa elimu ya usalama mtandao kwa Menejimenti ya Chuo cha Ufundi cha Arusha, Oktoba 17, 2022, jijini Arusha.

Mhandisi Wangwe amesema kuwa suala la usalama mtandao ni changamoto ya kidunia ambapo takwimu zinaonesha kila siku majaribio milioni 156 ya uhalifu kwa njia ya barua pepe au tovuti hutokea na majaribio milioni 16 hufanikiwa.

Ameongeza kuwa Serikali kupitia Wizara hiyo imeendelea kuimarisha usalama wa mtandao kwa kujenga mazingira wezeshi na mifumo imara ya kusimamia sera, sheria, kanuni na miongozo ya usalama wa mtandao pamoja na kutoa elimu kwa makundi yote katika jamii ili kupunguza mianya ya uhalifu wa mtandaoni.

“Usalama wa mtandao huanza na mtu binafsi, pamoja na juhudi nyingi zinazofanywa na Serikali, bado kila mtu analo jukumu la kuchukua tahadhari na kujilinda na uhalifu unaofanywa kwa njia ya mtandao”, Amesema Wangwe

Naye Mtaalamu wa Masuala ya Usalama Mtandao na Uchunguzi wa Kidijiti wa African ICT Alliance (AfICTA) kutoka Tanzania, Bw. Yusuph Kileo amesema kuwa, namba ya siri imara na madhubuti ni kitu cha kwanza na cha msingi za kujilinda na uhalifu wa mtandao lakini pia umakini na kuchukua tahadhari kutawaepusha watumiaji kuwa wahanga wa uhalifu wa mtandao.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Wangwe amewataka wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu cha Arusha (IAA) kutafakari mara mbili kabla ya kuweka chochote mtandaoni ili kujiepusha na matukio ya udhalilishaji na utapeli ambayo yanaweza kuathiri maisha yao ya baadae.

Akijibu maswali mbalimbali ya wanafunzi chuoni hap oleo oktoba 17, Mhandisi Wangwe ametolea ufafanuzi masuala kadhaa ikiwa ni pamoja na huduma ya bure ya kutafuta simu iliyoibiwa na umakini wa Serikali wa kujiridhisha kabla ya kuzifungia namba za simu zilizoripotiwa kufanya uhalifu kupitia namba 15040.

Mapokeo ya Elimu ya Usalama mtandao kwa Menejimenti ya Chuo cha Ufundi cha Arusha na wanafunzi wa Chuo cha IAA yamekuwa ni mapokeo chanya ambapo kwa nyakati tofauti wamekiri kuwa elimu iliyotolea imewafungua katika maeneo mengi sana na matamanio yao ni Wizara kuendelea kutoa mafunzo haya mara kwa mara na kuyafikia makundi yote ya kijamii.

 

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.