• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wazazi Mtaa wa Mazengo washauriwa kulea watoto katika maadili

Imewekwa tarehe: August 27th, 2023

Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE

WAZAZI wa Mtaa wa Mazengo Kata ya Chang’ombe wametakiwa kijikita katika malezi ya watoto ili wawe na maadili mema yatakayowawezesha kuwa raia wema na wawajibikaji katika jamii.

Kauli hiyoilitolewa na Afisa Ustawi wa Jamii wa Kata ya Chang’ombe, Debora Kanuya alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa Mazengo kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kufanyika katika Ofisi ya CCM Tawi la Chang’ombe Magharibi jijini Dodoma.

Kanuya alisema “ninawaomba sana akina mama wa Mtaa wa Mazengo, tuwe na maneno mazuri kwa watoto wetu ili watoto wanapokuwa wawe wanafahamu maneno mazuri, wasiwe na maneno ya matusi na maneno ya mtaani. Lakini pia kuna baadhi ya akina mama ambao wamekuwa wakipiga sana watoto wao na kutoa lugha ya matusi. Unakuta baadhi ya kina mama wametelekezwa kwa hiyo zile hasira za kutelekezwa wanazihamishia kwa watoto, huo ni ukatili. Niwaombe sana wanawake wenzangu tujikite katika malezi bora ya watoto wetu ili waje kuwa viongozi na raia wema kama sisi. Sisi tusingepata malezi bora tusingekuwa katika nafasi hizi na kuweza kuongea nanyi”.

Aidha, alikemea tabia ya baadhi ya wanawake wanaokunywa pombe kupindukia. “Ndugu zangu kuna akina mama ambao wanakunywa sana pombe. Kinachosikitisha zaidi wanakwenda na watoto vilabuni. Kina mama wengine hawana muda na watoto wao, watoto wanashinda wakiwa wachafu, wakiwa na njaa. Tuwatunze watoto wetu ili baadae pia watutunze” ailisema Kanuya kwa uchungu.

Kwa upande wake Katibu wa Hamasa na Chipukizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma, Nasra Seif alisema kuwa jamii inatakiwa kuwalea watoto katika maadili mema ili kuwa na taifa imara lenye watu wanaowajibika. “Siku hizi kumekuwa na tatizo kubwa sana la ukatili wa kijinsia kwa watoto. Twende tukawalee watoto kwa maadili na nidhamu” alisema Seif.

Mkazi wa Chang’ombe, Juma Shaban alisema kuwa changamoto kubwa kipindi hiki ni malezi ya watoto. Watoto wanaanchiwa kujilea na kulelewa na makundi rika jambo linalosababisha kukuwa bila maadili yaliyo mema kwa jamii.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.