• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wazazi na Wanafunzi watakiwa kujikita katika maombi

Imewekwa tarehe: November 18th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WAZAZI na wanafunzi wameshauriwa kujikita katika maombi ili Mungu aweze kufungua ufahamu utakaowawezesha wanafunzi kutumia maarifa waliyoyapata kipindi wakiwa shule katika kufaulu mitihani yao na kuwa raia wema.

Ushauri huo ulitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akiongelea umuhimu wa maombi kwa wanafunzi wanaofanya mtihani wa taifa wa kidato cha Nne ofisini kwake.

Fungo alisema “maombi ni ile hali ya mtu kuzungumza na muumba wake. Watoto wetu waliopo shuleni wengi wanaimani na wanamuamini Mwenyezi Mungu, hivyo wanafahamu kuwa Mungu yupo. Mtu anapofanya maombi anaeleza mambo ambayo anahitaji ili Mungu amsaidie. Kipindi hiki cha mtihani wa taifa wa kidato cha Nne ni muhimu kwa wazazi kufanya maombi kwa ajili ya watoto wetu na watoto kwa sehemu yao wakamuomba Mungu awasaidie”.

Alisema kuwa vitabu vya dini vinaelezea wazi umuhimu wa kuitafuta elimu kwa nguvu na kuishika sana. “Mungu ndiye anatupa uzima, Mungu ndiye anatupa afya, Mungu ndiye anayetusaidia kwa kila jambo. Hivyo, ni muhimu kurudi kwa Mungu kumuomba ili awasaidie watoto wetu waweze kufanya vizuri katika mitihani yao. Wafanye vizuri kwa ajili ya faida yao na kwa ajili ya taifa lao. Sisi wazazi tunawategemea wao kuja kushika nafasi zetu ambao tayari tupo kazini. Tunawategemea kuja kushika nafasi za wafanyabiashara na nafasi mbalimbali kwa ajili ya ustawi wa familia zao na taifa lao” alisema Fungo.

Mkuu huyo wa Kitengo cha TEHAMA alisema kuwa kutokana na umuhimu huo, serikali inatoa fedha nyingi kugharamia elimu kwa lengo la kuwasaidia wananchi wake wapate elimu hiyo bila malipo ili kila mtoto apate fursa hiyo adhimu. Alisema kuwa wazazi wana wajibu wa kuunga mkono juhudi za serikali kuhakikisha watoto wanasoma na kufikia malengo yao na malengo ya taifa.

“Wanapoendelea na mitihani hii tunawatakia heri na mwenyezi Mungu awe pamoja nao awasaidie wakumbuke kila walichojifunza, Mungu awape hekima, ufahamu na maarifa waweze kufanya vema kwa faida ya taifa letu na faida ya familia zetu” alisema Fungo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.