• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wazazi tuwajengee watoto uwezo kujiamini, kujieleza

Imewekwa tarehe: October 13th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WAZAZI katika Wilaya ya Dodoma wametakiwa kuwajengea uwezo wanatoto wao ili waweze kujiamini na kujieleza ili waweze kutoa taarifa za vitendo vya ukatili wa kijinsia vinapojitoleza ili waweze kuwa salama.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alipokuwa akifunga mashindano ya mdahalo kwa shule za sekondari zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma yaliyofanyika katika shule ya sekondari Dodoma.

Shekimweri alisema kuwa watoto wamekuwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa kijinsia kutokana na kutokuwa na uwezo wa kujieleza. “Kama watoto wetu tukawafundisha na kuwajengea kujiamini na kujenga hoja ni ngumu mtu mwenye dhamira mbaya kufanya vitendo vya ukatili wa kijinsia” alisema Shekimweri.

Aliongeza kuwa tafiti zinaonesha kuwa miongoni mwa wanaosababisha ukatili wa kijinsia ni ndugu wa karibu wa familia. “Unakuta mjomba, baba mkubwa ndio wanaofanya ukatili kwa watoto. Hivyo, watoto wakiwa na kujiamini wataweza ‘kuraise voice’ kwamba vitendo hivyo havifai” alisema Shekimweri.

Kwa upande wake Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwalimu Upendo Rweyemamu alisema kuwa mashindano ya mdahalo kwa shule za

Halmashauri ya Jiji la Dodoma ngazi ya wilaya ni jambo jema. Aidha, aliagiza mashindano hayo yafanyike kwenye ngazi ya shule kati ya darasa na darasa ili kuwajengea wanafunzi uwezo wa kuzungumza na kuandika kwa lugha ya kiingereza.

Akiongelea umuhimu wa mdahalo katika taaluma, Rweyemamu alisema kuwa midahalo inamjengea mwanafunzi ujasiri wa kujielezea, kujenga hoja, inamuongezea misamiati ya lugha ya kiingereza, inamjengea ujasiri pia inaongeza ufaulu kwa wanafunzi.

“Tunaenda kuongeza ufaulu katika shule zetu sababu wanafunzi wanaenda kuwa vizuri kwenye lugha ya kiingereza, mwanafunzi anaweza akawa ameelewa swali lakini hana misamiati yakutosha ataishia kujua kichwani mwake lakini atashindwa kuweka kwenye maandishi kupitia midahalo mwanafunzi ataongeza misamiati na kumudu masomo yake pamoja na mitihani anayoulizwa kwa lugha ya kiingereza”, alisema Rweyemamu.

Mratibu wa mashindano ya mdahalo huo, Mwalimu Malick Masoud alisema kuwa mada zilizofanyiwa mdahalo huo zinalenga kupinga ukatili wa kijinsia. Alisema kuwa lengo ni kuona namna wanafunzi wanavyoshindwa kufikia malengo yao kutokana na ukatili wa kijinsia na namna ukatili huo unavyowaathiri.

“Watoto wanashindwa kufikia malengo yao kutokana na mambo ya ukatili wa kijinsia. Mashindano haya yana lengo mahususi la kuwasaidia wanafunzi kuchangamsha akili zao kwasababu wanakutana na wanafunzi kutoka shule mbalimbali na wenye uwezo tofauti, lakini pia yatasaidia kujenga uelewa wa masuala ya ukatili wa kijinsia na umuhimu wa utunzaji wa mazingira kutokana na mada walizozizungumzia katika mdahalo” alieleza Masoud.

Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mnadani, Haruna Jumaa alishauri kwa wanafunzi wenzake kuchukua hatua wanapofanyiwa vitendo vya ukatili. Alisema kuwa ukatili hauwezi kuwa ukatili kama muathirika hataweza kutoa taarifa na hiyo hutokana na kutokujiamini. “Ukiona kitendo kinataka kutokea au kimekwisha kutokea toa taarifa kwa vyombo husika au hata kwa waliokuzidi umri ili waweze kupata namna ya kukusaidia” alisema Jumaa.

Mashindano hayo ya mdahalo yalianza tarehe 1 Oktoba, 2022 yakijumuisha shule 16 zilizopo ndani ya Jiji la Dodoma yalifikia ukomo jana na shule ya sekondari Miyuji kuibuka mshindi wa jumla.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.