• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wazazi wahimizwa kupeleka watoto kupata Chanjo ya Surua na Rubella

Imewekwa tarehe: February 15th, 2024

WIZARA ya Afya kwa ushirikiano na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma imefanya uzinduzi wa kampeni ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa Surua na Rubella inayotarajiwa kuanza kutolewa Februari 15 hadi 18, 2024 kwa watoto wenye umri kuanzia miezi 9 hadi miaka mitano(5).

Kampeni hiyo imezinduliwa rasmi kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa jengo la Mkapa Jijini Dodoma na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule.

Senyamule amewasisitiza wazazi wote wenye watoto wenye umri unaostahili kujitokeza kwa kwa wingi kuwapeleka watoto wao wapate chanjo hiyo.

“Tumekua tukipata chanjo hizi mara kwa mara kutokana na uhitaji ili kuepuka madhara yanayotokana na ugonjwa wa Surua. Nitoe Wito kwa wazazi wote wenye watoto wenye umri unaostahili kujitokeza kwa wingi wapate chanjo hiyo. Chanjo zimeandaliwa vizuri na kwa uhakika.

“Wakati wote Dodoma tumekua tukifanya vizuri kwenye chanjo hivyo hata wakati huu nitoe shime tufanye hivyo kwani Dodoma tumepewa heshima ya kufanya uzinduzi wa kampeni hii kitaifa siku ya Ijumaa. Tuwapeleke watoto kwenye vituo vya afya kwa tarehe zilizopangwa. Kwa pamoja tunaweza kutokomeza Surua na Rubella” Amesisitiza Senyamule.

Akitoa wasilisho la namna Mkoa uliyojipanga kufanikisha zoezi hili, Afisa chanjo Mkoa wa Dodoma Francis Bujiku, amesema;

“Tunatarajia kutoa chanjo hii kwa walengwa 426,964 na tayari dozi 469,660 zimeshasambazwa kwenye vituo vyote vya kutolea huduma hiyo ambavyo ni 543. Mradi huu imegharimu kiasi cha Shilingi 452,682,000.00 zilizotolewa na Shirika la GAVi chini ya Wizara ya Afya. Mpaka Sasa chanjo na vifaa vyote vimeshasambazwa”Bujiku.

Ugonjwa wa Surua na Rubella huambukizwa na virusi vinavyosambaa kwa njia ya hewa na dalili zake ni pamoja na homa, kikohozi, macho kuwa mekundu, vipele vidogo vidogo mwilini na n.k Magonjwa haya yanakingwa kwa chanjo tu. Chanjo hizi zinatarajiwa kutolewa kwenye vituo vya afya kwa huduma ya mkoba pamoja na klinik tembezi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.