• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wazazi, Walezi watajwa ukatili wa kijinsia

Imewekwa tarehe: March 8th, 2020

MWENYEKITI wa dawati la jinsia mkoani Dodoma, Theresia Mdedemi amewaja wazazi na walezi kuwa ni moja kati ya watu wanaofanya vitendo vya ukatili kuongezeka kutokana na usiri na matendo mengi kumalizwa kifamilia hali inayowafanya wahusika wa matendo hayo kuwa sugu.

Aliyasema hayo katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kimkoa katika uwanja wa Shule ya Msingi Mkonze wakati akitoa taarifa kwa mgeni rasmi Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Dodoma, Mhe. Felista Bura ambapo alitoa ripoti ya matukio ya ukatili wa kijinsia kwa mkoa wa Dodoma.

Mdedemi alisema kuwa, hiyo ndiyo changamoto kubwa wanayokumbana nayo katika dawati la jinsia na kuonekana kuwa ndio uzio wa kumalizika kwa tatizo la ukatili wa kijinsia, ambapo wazazi, walezi na jamii kwa ujumla wana mtazamo hasi wa  kuripoti matukio hayo na kuona kama familia itadharaulika hivyo kuyamaliza majumbani bila ya kuyaripoti polisi katika dawati la jinsia.

“Takwimu za kesi zilizoripotiwa kuanzia Januari hadi  Disemba kwa mwaka 2018 ni kesi 1,114. KUbaka kesi 303, kulawiti kesi 76, kukeketakesi 4, kutoa mimba kesi 13, kutelekeza watoto kesi 88, kutelekeza familia kesi 124,  shambulio la kudhuru mwili kesi 194, kuzini na maharimu kesi 9, kutorosha wanafunzi kesi 144,  mimba kwa mwanafunzi kesi 159.

“Kipindi cha Januari hadi Disemba mwaka 2019, ulikuwa na jumla ya kesi 1,138. Kubaka kesi 191, kulawiti kesi 79, kutoa mimba kesi 10, kutelekeza watoto kesi 58, kutelekeza familia kesi 162, shambulio la kudhuru mwili kesi 254, kuzini na maharimu kesi 3, kutorosha wanafunzi kesi 202, na kumpa mimba mwanafunzi kesi 179”  alisema mwenyekiti huyo.

Mbali na changamoto hiyo pia, ametaja baadhi ya visababishi ambavyo vinapelekea ongezeko la takwimu hizo kwa mwaka 2019 tofauti na ilivyokuwa kwa mwaka 2019, kuwa ni pamoja na kushindwa kuyafikia maeneo ya pembezoni.

“Tunashindwa kuyafikia maeneo ya pembezoni kutokana na changamoto za rasilimali fedha na vifaa. Kutokana na hali hiyo tunashindwa kuandaa makongamano, vipeperushi, majarida, na semina ambavyo vingeweza kutusaidia kufikisha ujumbe haraka kwa jamii hali inayopelekea jamii kuwa na uelewa mdogo juu ya makosa ya ukatili, badala yake tunasubiria mialiko kutoka kwa wadau pekee.

“Aidha, ongezeko la wasichana wadogo kupelekwa mijini kwa ajili ya kufanya kazi za majumbani ambapo wengi wao huishia kufanyiwa vitendo wa kikatili. Lakini kutokana na mazingira yanayotumika, wengi hushindwa kuwa wakweli katika kueleza uhalisia wa yale wanayokumbana nayo na mwisho wa siku huishia kuvumilia ili waendelee kukaa mjini. Hivyo niwaombe tu tuvunje ukimya ukifanyiwa ukatili njoo uripoti bila kuangalia aliyekufanyia ni nani”, alisisitiza.

Alimetoa wito kwa wazazi, walezi, wadau jinai na wasimamizi wa sheria wawe makini katika usimamiaji wa sheria zinazomkandamiza mwanamke, na kuhakikisha wote wanaohusika katika ukiukaji wa sheria hizo kukamatwa, kufunguliwa mashtaka, kuhukumiwa na kuadhibiwa kisheria kwa mujibu wa sheria ili iwe fundisho kwa wenye tabia za kukiuka na kuzivunja sheria kwa kutekeleza ukatili wa kijinsia.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.