• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wazazi, wasichana watakiwa kuzungumzia hedhi

Imewekwa tarehe: May 28th, 2020

WAZAZI na walezi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kuwa mstari wa mbele kuwatengenezea watoto wa kike mazingira rafiki wanapokuwa katika mzunguko wa siku za hedhi ili wasivuruge ratiba za masomo yao.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwalimu Upendo Rweyemamu alipokuwa akiongelea nafasi ya wazazi na walezi katika kumsaidia mtoto wa kike kuendelea na masomo anapokuwa katika mzunguko wa hedhi.

Mwalimu Rweyemamu amesema kuwa wazazi na walezi wanalo jukumu la msingi la kuwaelekeza Watoto wa kike kabla hawajaanza na wanapoanza mzunguko wa hedhi. “Wazazi, walezi na jamii kwa ujumla wanatakiwa kuwa mstari wa mbele kuwahamasisha watoto wa kike kutokupoteza vipindi vya shule wanapokuwa katika mzunguko wa hedhi. Lazima wawatengenezee mazingira sahihi Watoto wa kike kuelewa hali watakayokuwa nayo wakati wa hedhi” alisema Mwalimu  Rweyemamu. Baadhi ya watoto wa kike wanapokuwa katika mzunguko wa hedhi hutumia siku nne hadi tano, hivyo kila mwezi mtoto wa kike anajikuta akipoteza wiki nzima ya kutohudhuria masomo, aliongeza. “Mzunguko huo unamfanya mtoto wa kike kupoteza siku nyingi za masomo. Wakati wenzake wanaendelea na masomo, wao wanakuwa wanakikosa masomo, na walimu hawawezi kurudi nyuma” aliongeza Mwl. Rweyemanu.

Aidha, aliwataka walimu katika Halmashauri ya Jiji kukumbuka kuwa Watoto wa kike wanapokuwa shuleni wanakuwa chini yao. “Walimu ndiyo wazazi kipindi watoto wa kike wanapokuwa shuleni. Hivyo, wanawajibu wa kuwaandalia sehemu maalum kwa ajili ya kujisitiri yenye usiri na usafi wa kutosha. Walimu wakiwatengenezea mazingira hayo, kutawawezesha watoto wa kike kuwa huru wakati wa masomo” aliongeza Mwalimu Rweyemamu.

Kwa upande wa watoto wa kike, aliwataka kufahamu kuwa mzunguko wa hedhi siyo ugonjwa, bali ni utaratibu ambao kila mwanamke lazima aupitie katika utimilifu wake. “Nichukue nafasi hii kuwashauri watoto wa kike wajitahidi wasibaki nyumbani, ili waweze kuhudhuria vipindi shuleni, ni kweli kuna maumivu wanayopitia kama kuumwa tumbo, kichwa na mgongo. Zipo njia za kawaida kupunguza maumivu hayo kama kunywa maji ya moto au kunywa maji mengi. Maumivu yanapozidi ni vizuri kufika katika vituo vya kutolea huduma za afya” alisisitiza Mwalimu Rweyemamu. Dhamira ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni kuona Watoto wote wa kike wakisaidiwa kipindi chote wanapokuwa katika mzunguko wa hedhi ili waweze kuhudhuria masomo yao katika juhudi za serikali kukuza na kuimarisha sekta ya elimu.  

Ikumbukwe kuwa tarehe 28 Mei kila mwaka ni siku ya hedhi salama duniani ambapo jamii hujadili jinsi ya kutatua changamoto zinazowakabili wanawake na Watoto wa kike wanapokuwa katika mzunguko wa hedhi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.