• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wazazi watakiwa kufatilia mienendo ya watoto wao

Imewekwa tarehe: November 11th, 2022

Na. Theresia Nkwanga. DODOMA

AFISA Elimu Msingi  Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prisca Myalla amewataka wazazi kuwa karibu na walimu, kufatilia mienendo ya tabia za watoto wao ili kuwalinda dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Hayo ameyasema alipokutana na wazazi wa Kata ya K/Ndege katika shule ya msingi Mlimwa A iliyopo jijini Dodoma, kwaajili ya  kuzungumza maswala mbalimbali ya malezi ya watoto, Lishe na namna ya kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye Kata ya K/Ndege.

Aidha, amewataka wazazi kufanya jukumu lao la malezi ya watoto nakuacha visingizo vyakushindwa kuwalea kwa sababu ya kutafuta fedha za kuendeshea  Maisha.

‘’Tunapaswa kuwaelekeza hiki ni  kizuri hiki ni kibaya, turudi kwenye misingi ya malezi ya watoto tufatilie mienendo ya watoto kupitia walimu wanaowafundisha hasa walimu wa darasa, fahamu marafiki zake ni kina nani, fahamu akiwa shuleni anatabia zipi na akiwa nyumbani anatabia gani na vilevile fahamu ratiba ya vipindi vya shule vinaisha saa ngapi. Niwasihi kina mama kuwaandaa watoto vile unavyotaka awe ni jukumu lako ukishirikiana na baba tuache visingizio vya kutafuta pesa huku tukiwaacha watoto wetu wanaangamia nakufanyiwa matendo maovu,” alisema Myalla

Akielezea namna ambavyo tunaweza wakinga watoto na vitendo vya ukatili Afisa Ustawi Wa Jamii Halmashauri, Recho Balisija alisema wazazi wanatakiwa kujenga tabia ya kukaa na kuzungumza na watoto wao,kushirikiana nao na kujenga urafiki na watoto ili wawe huru kuwataarifu pale wanapopitia changamoto yoyote na kuripoti wanapoona viashiria vya ukatili

‘’Turudi kwenye dini tuwalee watoto katika misingi ya dini, dini ni msaada mkubwa kwenye malezi ya watoto wetu, hakuna dini inayoruhusu ukatili tubebe watoto tuwapeleke kanisani  tuwe na utaratibu wa kusali nao jioni, mtoto akilelewa katika imani atajifunza swala la ukatili ni dhambi Mungu hapendi’, aliongezea Basilija.

Naye, Afisa Maendeleo Dawati la Jinsia na Watoto Krista Kayombo, aliwaomba wazazi warudi kwenye mila na desturi zao za zamani wawarithishe watoto mila zilizo njema ili kukikomboa kizazi hiki cha sasa kinachoangamizwa na utandawazi.

‘’Wazazi wetu wazamani  walikua na mila na desturi binti akivunja ungo anatakiwa kujistiri na haruhusiwi kuingia hovyo kwenye vyumba vya watoto wa kiume ila siku hizi watoto wakike wanavaa nguo zenye kuonesha maungo yao mbele za baba na kaka zao,” alisema Kayombo

Kwa upande wake James Magawa mzazi aliyehudhuria kikao hicho, aliwashauri  wazazi kuwalea watoto katika misingi ya dini pia kuweka utaratibu wa kusali nao jioni ili kuwajenga watoto katika misingi ya kidini toka wakiwa wadogo alimalizia kwa kumshukuru Afisa elimu msingi kwa elimu aliyowapatia na kumuomba ikiwezekana hii elimu itolewe kuanzia ngazi ya shule.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.