• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wazee ni hazina, hekima ipo kwao

Imewekwa tarehe: October 1st, 2019

WAZEE ni hazina kutokana na mchango wao katika kupigania uhuru na kutengeneza dira ya maendeleo kwa taifa.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Patrobas Katambi aliyekuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wazee duniani ngazi ya Wilaya yaliyofanyika katika uwanja wa Nyerere square jijini Dodoma leo.

Katambi alisema “Umoja wa mataifa uliona umuhimu na mchango wa wazee duniani. Taifa lolote lililoendelea liliendelezwa na vijana wa wakati ule ambao ndiyo wazee wa sasa. Wazee ndiyo walipigana vita na kuleta uhuru. Wazee mnawajibu wa kushauri katika ngazi mbalimbali. Hata kwenye makanisa kuna wazee washauri. Ninyi ndio mnaotoa dira ya nchi hii”.

Serikali inatambua umuhimu wa wazee kama kundi muhimu katika jamii. Rais Dkt. Magufuli kwa kutambua umuhimu wa wazee alianzisha wizara inayogusa moja kwa moja masuala ya wazee ili kulinda stahili za wazee, alisema. “Serikali inaendelea kusisitiza na kutoa huduma bora kwa wazee. Katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, jumla ya vitambulisho 10,290 vimetolewa kwa wazee kwa ajili ya matibabu katika kata mbalimbali. Aidha, wazee 4,551 wamepatiwa misamaha ya tiba katika vituo vya afya” alisema Katambi.

Akiongelea hali ya tiba katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mkuu wa Wilaya alisema kuwa hali ya tiba ni nzuri. “Halmashauri imekuwa ikifanya vizuri katika kusimamia huduma za afya. Viongozi wote wakiongozwa na Mkurugenzi wa jiji wanafanya kazi kubwa kuhakikisha maslahi ya wazee yanalindwa” alisisitiza mkuu wa Wilaya.

Kwa upande wake, Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mhe. Emmanuel Chibago alisema “sehemu isiyokuwa na wazee hakuna hekima. Hekima ipo na wazee. Wazee ndiyo mnatakiwa kutulea sisi. Tunapoenda tofauti mtuite na kuturudisha kwenye mstari”. Aidha, aliwataka wazee hao kuwa na imani na serikali yao.

Katika risala ya wazee iliyosomwa na Katibu msaidizi wa baraza la wazee Wilaya ya Dodoma mjini, Veronica Mvutekule alisema kuwa wanaiomba serikali kuchukua hatua kali kwa familia zinazotelekeza wazee wao kwenye huduma za matunzo na makazi. “Tunaomba serikali ifikirie kuwapa wazee pensheni na mikopo isiyokuwa na riba. Tunaiomba serikali ituondolee kodi ya ardhi. Sheria ya wazee itungwe pamoja na kanuni zake” alisema Mvutekule.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.