• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri amhakikishia Rais Samia kusimamia ujenzi wa miundombinu ya afya na kukamilika kwa wakati

Imewekwa tarehe: June 8th, 2022

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Innocent Bashungwa amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kuwa ujenzi wa miundombinu ya huduma za afya katika hospitali za Wilaya, vituo vya afya na zahanati zote nchini utakamilika kwa wakati na kwa ubora zaidi ili wananchi waendelee kupata huduma bora za afya kwa wakati.

Bashungwa amesema kuwa kufuatia maelekezo yaliyotolewa na Mhe. Rais kuwa hataki kuona majengo ya hospitali yaliyomalizika kujengwa hayatumiki na badala yake yanabaki kuwa maboma, OOfisi ya Rais - TAMISEMI inaenndelea kutekeleza maagizo hayo akisisitiza kuwa ukamilishaji wa majengo hayo ya vituo vya afya unaambatana na ununuzi wa dawa, vitendanishi na vifaa tiba pamoja naa ajira za watumishi watakaotoa huduma katika vituo hivyo.

Hayo yamesemwa leo tarehe 8 Juni, 2022, katika ziara ya Rais Samia Wilayani Biharamuro, Mkoani Kagera.

"Mhe. Rais ulituagiza Ofisi ya Rais - TAMISEMI kuwa hutaki kuona majengo ya hospitali yanabaki kuwa maboma, lakini pia ulituelekeza ujenzi wa hospitali hizi, vituo vya afya na zahanati lazima ukamilike ili wananchi wapate huduma, nikuhakikishie Mhe. Rais ujenzi wa miundombinu hii itakamilika kwa wakati na ubora zaidi" amesema Bashungwa.

Aidha, Waziri Bashungwa amemshukuru Mhe. Rais kwa kuwekeza fedha kwa ajili ya uboreshwaji wa miundombinu ya kutolea huduma za afya ya msingi, barabara na miundombinu ya elimu ya msingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Biharamuro, Bashungwa amesema mindombinu hii inakwenda kuboresha maisha ya wananchi wa Biharamuro na Mkoa wa Kagera kwa ujumla.

Kwa upande mwingine, Bashungwa amesema kutokana na maelekezo aliyotoa Mhe. Rrais kuhusiana na zao la Buni ambalo kwa asilimia kubwa linalozalishwa Mkoani Kagera, maelekezo hayo yameleta matumaini makubwa kwa wakulima na wafanyabiashara wa zao hilo kwa kuwa bei ya buni imepanda hadi kufikia shilingi 3,720 kwa kilo. 

"Muelekeo uliotoa Mhe. Rais katika zao la kahawa, matumaini ni makubwa, mwaka jana ulifanyika mnada wa zao la buni aina ya Radika limeuzwa kwa bei ya 3,720 haijapata kutokea" alisisitiza Bashungwa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.