• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri TAMISEMI ataka chombo kusimamia miradi mikubwa

Imewekwa tarehe: April 13th, 2021

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Ummy Mwalimu ameliagiza Jiji la Dodoma kuunda chombo maalumu kwa ajili ya kusimamia uendeshaji wa miradi mikubwa ya kimkakati waliyonayo ikiwemo kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani na nchi za nje cha Jijini Dodoma.

Pia ametaka mfumo wa utoaji huduma kituoni hapo uendelee kuwa rafiki kwa  wateja, wajasiliamali, wafanyabiashara na wananchi wote kwa ujumla wanapopata huduma.

Waziri Ummy ametoa maagizo hayo Aprili 12, 2021 wakati alipofanya ziara katika kituo kikuu cha mabasi kilichopo eneo la Nanenane Kata ya Nzuguni Jijini hapa, ambapo alisema lazima kiundwe chombo kwa ajili ya kuendesha miradi hiyo ili iweze kuleta tija kwa nchi kama malengo yalivyokusudiwa.

“Kuna muongozo maalumu wa uendeshaji wa miradi hii, ili ilete tija, mimi nadhani kiundwe chombo maalumu cha kuendesha miradi hii ili tufikie lengo tulilokusudia, tunataka miradi hii izalishe mapato ili tukajenge shule, hospitali” alisema Waziri Ummy.

Alisema Serikali imewekeza zaidi ya shilingi bilioni 24 katika mradi huo wa stendi hivyo mradi huo usimamiwe kikamilifu ili utoe huduma bora, huku akitaka mabasi yote yaanzie na kumalizia safari zake katika kituo hicho.

Waziri alisema Serikali ya awamu hii ikiongozwa na Rais wa sita wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  itaendelea kujali wafanyabiashara wadogo na kutaka wafanye biashara zao kwa amani na kwa kufuata sheria na taratibu wanazowekwa na mamlaka husika.

Kwa upande wake,  Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru alisema mpaka sasa mradi huo unasimamiwa na Jiji lakini wapo katika mchakato wa kuunda chombo kitakachosimamia na kuendesha miradi mikubwa ya kimkakati ya Jiji hilo ikiwemo kituo hicho, Soko Kuu la Job Ndugai na Hoteli ya kisasa yenye ghorofa 11 ya Dodoma City Hotel iliyopo katikati ya Jiji na wameshapeleka andiko ofisi ya Mkoa ili kubadilisha mfumo wa uendeshaji wa mradi huo na miradi mingine iliyopo katika jiji la Dodoma.

Naye meneja wa kituo hicho Abeid Msangi alisema kituo hicho kilianza kutoa huduma Juni 8, 2020 na kinauwezo wa kuhudumia mabasi mia moja (100) kwa wakati mmoja, na mpaka sasa tayari wameshakusanya shilingi milioni mia sita themanini (680,000,000) tangu kituo hicho kianze kufanya shughuli zake.

Ameongeza kuwa “kutokana na changamoto ya wafanyabiasha kutopanga maeneo yote ya biashara, tumeamua kushusha kodi ya pango kutoka shilingi elfu kumi na tano (15,000) ya awali kwa mita ya mraba hadi kufikia elfu kumi (10,000) ili tuwavutie wateja wengi zaidi kufanya biashara” alisema Msangi.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.