• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri Jafo aridhishwa na ujenzi wa Hospitali ya Uhuru

Imewekwa tarehe: July 17th, 2019

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe Selemani Jafo amefurahishwa na hatua za awali za ujenzi wa Hospitali ya Uhuru inayojengwa katika eneo la Chamwino Mkoani Dodoma kwa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli.

Mhe. Jafo amesema amefanya ziara  maalumu ya kukagua ujenzi wa Hospitali hii ya Uhuru tarehe 15 Julai 2019 baada ya kufika katika eneo hilo  mnamo mwezi Juni  na kutoridhishwa  na hali aliyoikuta, ujenzi ulikuwa haujaanza na hata eneo lilikuwa halijasafishwa.

”Nilikuja hapa Juni 19 kukagua eneo hili sikuridhishwa baada ya kukuta ujenzi haujaanza, ndio maana nikatoa maelekezo kwamba ujenzi uanze mara moja kwa kutumia kikosi maalumu cha Jeshi ili kutimiza azma ya Mhe. Rais katika kutoa huduma bora za Afya karibu na wananchi, leo naona  tayari wenzetu wa Suma JKT wameshaanza kazi hili limenifurahisha,” amesema Mhe Jafo.

Hivi ndio tunavyotakiwa tufanye kazi sio mnapewa maelekezo halafu mnaanza kujivuta vuta kufanya vikao visivyoisha hiyo haipendezi kwa sababu mnawacheleweshea wananchi huduma, aliongeza Jafo.

Nimefurahi zaidi kuona  eneo lote la Ekari 40 limeshasafishwa ikiwemo kujenga uzio pamoja na ofisi za wafanyakazi wajenzi, pia vifaa vimeshaanza kufikishwa katika eneo hili la Hospitali na TBA wako wanaendelea na kazi yao ya usimamizi na ushauri hongereni kwa hilo alikazia Jafo.

”Kwa kweli leo nimeridhishwa na hatua ya awali ambayo tumefikia katika ujenzi wa Hospitali hii, na niwaombe wataalamu wangu kuacha kufanya kazi kwa mazoea na tunapotoa maagizo basi wayatekeleze kwa wakati, ni matarijio yetu hadi kufikia Januari, 2020 tutakua tumeshakamilisha ujenzi huu,” alisisitiza Mhe. Jafo.

Kwa upande wake Mhandisi kutoka Wakala wa Majengo Tanzania TBA, Mhandisi Daniel Mwakasungura amesema Hospitali hiyo ya Uhuru itakuwa ni ya gorofa moja na itatumia ramani ya Hospitali ya Tunduma iliyoboreshwa.

“Ramani iliyopendekezwa ambayo ni ya Hospitali ya Tunduma tunaendelea kuiboresha kulingana na mahitaji na viwango vya Hospitali ya Uhuru na sisi kama TBA tutasimamia suala la hili la ramani na kutoa ushauri wa mradi huu mpaka pale utakapokamilika” Alisema Mwakasungura.

Akizungumzia bajeti ya mradi mzima Mwakasungura amesema fedha iliyotengwa ambayo tumeingia mkataba na Suma JKT ni Shilingi Bilioni 3 ambazo zitajenga majengo yote yanayohitajika  na tunatarajia mradi huu utakamilika baada ya miezi sita kama ambavyo tulievyoelekezwa,” amesema Mwakasungura.

Nae Mhandisi wa Suma JKT, Luteni Kanali Onesmo Njau amesema walikabidhiwa jukumu la ujenzi huo Juni 19 mwaka huu na tayari washatekeleza maelekezo kutoka kwa Mhe. Jafo ikiwemo kuandaa ofisi, sehemu za kuishi kwa watendaji na muda sio mrefu wataanza ujenzi ili kukamilisha mapema kama ilivyoelekezwa.

Hospitali hiyo inajengwa baada ya Rais Magufuli kuelekeza kufanya hivyo katika sherehe za Uhuru mwaka 2018 ambapo alifuta sherehe hizo na kupeleka Fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya sherehe hizo kujenga Hospitali ya Uhuru mkoani Dodoma.

Chanzo: tovuti ya OR-TAMISEMI (www.tamisemi.go.tz)


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.