• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri Jafo asifu Jiji la Dodoma kuwa safi

Imewekwa tarehe: July 30th, 2022

Na. Dennis Gondwe na Sifa Stanley, DODOMA

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira, Selemani Jafo ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa juhudi zake za kuliweka jiji safi.

Pongezi hizo alizitoa mapema leo aliposhiriki zoezi la usafi pamoja na wananchi katika Soko la Bonanza Kata ya Chamwino Halmashauri ya Jiji la Dodoma

“Watu wa hapa mnafanya usafi kweli, sio kwa kuigiza. Nimetembea maeneo yote katika Samaki, Ndizi, Viazi pamoja na Matunda nimekuta mmefanya usafi. Ninyi ni watu wa kuigwa ndani ya Tanzania. Hii inadhihirisha kuwa maagizo ya Rais, Mama Samia na Dkt. Isdory Mpango akiwa yeye ni Makamu wa Rais na akisimamia upande wa Mazingira na Waziri Mkuu, wamekuwa wakitoa maelekezo kuhusu Mazingira na kufanya usafi, wanabonanza nimeshuhudia kwamba ni wasafi sana” alisema Waziri Jafo.

Pia Waziri Jafo alitoa wito kwa wananchi wa maeneo mengine kuzingatia maelekezo ya Serikali kuu ya kuacha biashara zao kwa muda mfupi na kufanya usafi siku ya Jumamosi. Sambamba na hilo alisisitiza watu wa maeneo mengine kuiga mfano wa Dodoma wa kuendeleza utamaduni wa usafi na kutunza Mazingira ili kuendelea kuiweka Nchi katika hali ya usafi.

“Niwaombe maeneo mengine waige mfano wa Dodoma, na Mkurugenzi wetu jambo hili liendelee katika masoko mbalimbali. Nafahamu wiki iliyopita tulikuwa na ajenda kama hii Soko la Majengo, leo hii tupo Soko la Bonanza inawezekana huenda Jumamosi ijayo tutakuwa Soko la Mavunde. Hili linawezekana tuwe tunabadilika, jiji letu tunafahamu ndio Makao Makuu ya nchi sura ya nchi yetu inapatikana Dodoma. Lazima tuhakikishe tunafanya usafi. Mimi kama Waziri wa Mazingira Tanzania hapa nimeridhika mnatunza Mazingira wanabonanza” alisema Jafo.

Nae Mkuu wa Idara ya Mazingira na udhibiti wa taka ngumu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imekuwa na utaratibu wa kufanya usafi kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi na kuongeza kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imetenga kiasi cha shilingi milioni 38 kwaajili ya kuboresha Soko la Bonanza.

“Katika Jiji la Dodoma tumekuwa tukifanya usafi kwa maelekezo ya mkuu wa mkoa kila Jumamosi tumekuwa tukifanya usafi isipokuwa Jumamosi ya pili ya mwezi huwa tunaiacha kwaajili ya maelekezo ya serikali kuu watu kufanya mazoezi. Soko la Bonanza ni moja kati ya masoko masafi kama alivyosema Afisa Mtendaji Kata ya Chamwino na Halmashauri ya Jiji la Dodoma imekuwa ikiendelea kuboresha mahali hapa na tumetenga shilingi milioni 38 kwa mwaka huu wa fedha wa serikali ili kuboresha soko hili” alieleza Kimaro.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma atoa pongezi kwa Madiwani

    May 25, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Wananchi Kata ya Madukani washukuru kuboreshwa huduma za Afya, Zahanati ya Chikande

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.