• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri Jafo asifu Mradi Mifumo ya Sekta ya Umma - PS3

Imewekwa tarehe: September 17th, 2019

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo amesema Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma (Public Sector Systems Strengthening - PS3) umesaidia kudhibiti matumizi ya fedha na kuweka kumbukumbu sahihi za mapato katika vituo vya kutolea huduma.

Akizungumza na uongozi wa mradi huo, Jafo alisema umeimarisha mifumo ya TEHAMA ikiwemo iliyodhibiti matumizi ya fedha na kuweka taarifa sahihi za mapato katika vituo vya afya.

Ametoa mfano wa mfumo wa kielektoniki wa kuandaa mipango, bajeti na ripoti kwa Mamlaka ya Serikali za Mitaa (PlanRep), na kusema kuwepo kwa mfumo huo kumesaidia kuokoa Sh. bilioni nane zilizotumika kwa timu za bajeti za halmashauri wakati wa kukaa na kuandaa bajeti na kusafiri kwa ajili ya uwasilishaji rasimu za bajeti zao ngazi ya taifa.

"Kwa sasa hizo fedha zimeokolewa, kwani halmashauri zinatuma rasimu ya bajeti zikiwa katika maeneo ya kazi na kuifikia mikoani, hatimaye Tamisemi. Ikiwa kuna maboresho yanafanywa kupitia teknolojia," alieleza.

Kuhusu Mfumo wa Uhasibu wa Utoaji wa Taarifa za Fedha kwenye vituo vya kutolea huduma, Jafo alisema kwa sasa fedha zinazowasilishwa katika vituo vya afya na shule zimekuwa na uwazi, kwani pindi wanapozipokea hufanya matumizi kwa kuzingatia taratibu za fedha kupitia mfumo huo.

Kutokana na mafaniko hayo, alipongeza mradi huo. Aidha, alieleza kuwa pongezi hizo hawezi kuzitoa mikono mitupu hivyo kuwakabidhi vyeti vya kuthamini mchango uliotolewa katika ofisi ya TAMISEMI.

“Cheti kimoja ni kwa ajili ya Shirika la Misaada ya Maendeleo ya Kimataifa (USAID) ambao ndio wamekuwa wakitoa fedha na cheti kingine ni kwa ajili yenu PS3 ambao mmekuwa watekelezaji wa kazi za mradi huo,” alieleza.

Alisema ofisi yake inajivunia kushikirikiana na PS3 katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi kwa sababu kazi inayofanywa na mradi huo imewezesha kuwa na serikali yenye uwazi, maendeleo endelevu na ustawi wa pamoja.

Mkurugenzi wa mradi wa PS3, Dk Emmanuel Malangalila aliishukuru serikali kwa ushirikiano inaowapa wakati wote wa utekelezaji wa kazi za mradi huo.

Dk Malangalila aliongeza kuwa mradi huo unatekelezwa katika mikoa 13 Tanzania Bara lakini kazi zilizofanywa zimegusa mikoa yote 26 kutokana na uhitaji na umuhimu wa kazi za mradi katika kila mkoa.

PS3 inayofadhiliwa na USAID inafanya kazi katika mikoa 13 na halmashauri 93 Tanzania Bara ikiwa na lengo la kuimarisha huduma za umma kwa njia ya utawala bora, mifumo ya mawasiliano, fedha, rasilimali watu, pamoja na tafiti tendaji.

Chanzo: www.habarileo.co.tz


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.