• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

WAZIRI JAFO AZINDUA MFUMO WA TAARIFA ZA KIJIOGRAFIA (GIS)

Imewekwa tarehe: March 15th, 2019
  • Akemea suala la utumiaji wa fedha mbichi

Waziri wa TAMISEMI Mhe. Sulemani Jafo mnamo March 14, 2019 katika ukumbi wa NSSF uliopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji amezindua Mfumo wa Taarifa za Kijiografia (GIS) uliofadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia Mradi wa Kimkakati wa Ukuzaji wa Miji na Majiji Tanzania (TSCP).

Akihutubia katika ukumbi huo alisema mfumo huo utasaidia katika ukuzaji wa mapato kwa halmashauri na namna ya kuwahudumia wananchi waliopo katika Manispaa hiyo kutokana na mfumo huo kuwa na taarifa mbalimbali zitakazoanza kukusanywa kutoka kwa makazi yote, biashara na huduma za jamii zilizopo katika eneo husika.

Alisema Manispaa ya Kigoma/Ujiji ndio imekuwa sehemu ya kuandalia mfumo huo ikiwa imepangwa kutumika katika halmashauri nane zinazopitiwa na mradi wa TSCP na kufadhiliwa na Benki ya Dunia huku akiwataka watendaji kujifunza Mfumo huo na kuhakikisha wataalamu wa Tehama waliopo katika halmashauri zote nane wanatoa ushirikiano katika mfumo huo.

Halmashauri nane zinazopitiwa na Mradi wa Kimkakati wa Ukuzaji wa Miji na Majiji Tanzania (TSCP) ni Halmashauri za Majiji ya Dodoma, Mwanza, Mbeya, Arusha na Tanga, zingine ni Halmashauri za manispaa ambazo ni Ilemela, Kigoma-Ujiji na Mtwara-Mikindani.

Akiendelea kuhutubia aligusia suala la upotevu wa mapato kutokana na upotevu wa mashine za kukusanyia mapato (POS) huku akiasa halmashauri kuchukua hatua za kimaadili katika upotevu huo na kuonya halmashauri katika utumiaji wa fedha mbichi ambazo zinakuwa hazijafuata taratibu katika kufikia matumizi.

Naye Mhandisi Mussa Nati ambaye ni mhandisi na mtaalamu wa mfumo wa GIS kutoka Benki ya Dunia alisema mfumo huo tayari umeshaanza kutumika katika wilaya ya Kinondoni na umeleta tija katika ujenzi wa barabara na jinsi ambavyo hakukuwa na tatizo la migogoro ya fidia kwa wakazi. Aidha, alieleza kuwa umeweza kukuza mapato katika wilaya hiyo na ametoa rai mfumo huo utumike vizuri na kuulinda kupitia wataalamu waliopo.

Naye meya wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Mhe. Hussein Ruhava alishukuru kwa uzinduzi huo kufanyika katika manispaa hiyo huku akisema ni heshima kubwa ambayo serikali imeitoa na ameahidi kutoa ushirikiano na madiwani wote katika ukusanyaji wa mapato kutokana na mfumo huo na kuitaka serikali kuitazama zaidi manispaa hiyo kutokana na uwepo wa huduma duni zilizopo.

Naye mkuu wa wilaya ya Kigoma kwa niaba ya Mkuu wa mkoa ametoa salamu na kusema ofisi ya Mkuu wa mkoa itatoa ushirikiano kwa kusimamia na kuhimiza halmashuri kutumia mfumo huo kwa usahihi.

Waziri Jafo baada ya kumaliza mkutano huo katika ukumbi wa NSSF ambapo viongozi mbalimbali walihudhulia kutoka ofsi ya Mkuu wa mkoa, Wakuu wa wilaya zote za mkoani Kigoma, wakurugenzi wa Halmashauri, Meya wa manispaa ya Kigoma/Ujiji, Mkurugenzi wa Kigoma/Ujiji, Madiwani, wataalamu, wenyeviti wa mtaa pamoja na waandishi wa habari alifanya ziara katika eneo la Msimba lilipo dampo la taka la manispaa ambapo alitoa tamko kuanza kutumika kuanzia sasa.

Chanzo cha habari: Mhandisi Emmanuel Manyanga

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.