• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri Mkuu asifu Mfuko wa Mawasiliano, Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: April 30th, 2019

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ameipongeza Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kwa kutimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake na kuweza kuboresha Mawasiliano nchini.

Akizungumza katika kilele cha Maadhimisho ya miaka 10 ya UCSAF yaliyofanyika kwa siku nne katika Viwanja vya Nyerere Jijini Dodoma, Majaliwa alisema kuwa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote kwa kushirikiana na watoa huduma mbalimbali wa Mawasiliano Nchini wameweza kupata mafanikio mbalimbali ikiwemo kupeleka mawasiliano katika Kata 703, kwenye Vijiji 2501 na kuwafikia wananchi zaidi ya milioni 5 pamoja na Mfuko huo kuweza kuchangia zaidi Shilingi Bilioni 118 katika kuhakikisha mawasiliano yanafika kwa wananchi.

“Mfuko huu tangu kuanzishwa kwake umetumia Shilingi bilioni 118 kufikisha huduma ya mawasiliano kwa wananchi zaidi ya milioni tano, kwa hiyo napenda kuwahahikishia wananchi kuwa serikali itaendelea kupeleka mawasiliano maeneo yote ili kila mmoja aweze kunufaika na fursa hii” Alisema Majaliwa.

Majaliwa aliongeza kuwa, Mfuko umeweza kupeleka vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika Shule 500 nchini pamoja na kutoa mafunzo ya TEHAMA kwa Walimu zaidi ya 800 kwa lengo la kuwezesha wanafunzi kujifunza somo hilo kwa ufanisi mkubwa.

Aidha, Waziri Mkuu Majaliwa alimpongeza Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Devis Mwamfupe na Mkurugenzi, Godwin Kunambi kwa jitihada zao za kuboresha mazingira ya wajasiriamali kufanya kazi zao.

Alitoa pongezi hizo baada ya kusoma bango lililoandaliwa na wafanyabiashara wadogo ‘machinga’ wa Dodoma kupongeza juhudi za serikali ya awamu ya tano.

“Pongezi kwa Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mkurugenzi na Waheshimiwa Madiwani kwa kusimamia vizuri biashara katika Jiji la Dodoma” Alisema Majaliwa.

Majaliwa alisema kuwa wajasiriamali wa Dodoma wanapongeza juhudi za Rais Mhe. Dkt. John Magufuli za kuboresha mazingira ya wajasiriamali kutekeleza majukumu yao katika Jiji la Dodoma kutokana na uongozi mzuri wa viongozi wa Halmashauri hiyo.

Vilevile, Mhe. Waziri Mkuu aliwataka wafanyabiashara hao kufanya biashara zao katika mazingira yanayokubalika.

“Machinga hakikisheni mazingira mnayofanyia biashara yanakuwa safi na wala msikae maeneo ambayo siyo rafiki kwa wateja wenu” alisema.

Kuhusu upimaji wa Afya, Waziri Mkuu aliwataka wananchi wa Dodoma kujitokeza na kupima Afya zao ikiwemo hali ya Maambukizi ya Virusi vinavyosababisha Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI) ili kupata matibabu mapema.

“Kila Mtanzania anawajibu wa kupima ili kutambua Afya yake na hii ni kampeni endelevu, nenda kituo cha afya kupima ili ujue afya yako…tunataka Watanzania wote tuwe tumefikia asilimia 90 ifikapo mwaka 2020. Watanzania watakaogundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya UKIMWI wawe wameanza dawa za kufubaza virusi hivyo” alisema  Majaliwa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.