• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri Mkuu Majaliwa mgeni rasmi vita dawa za kulevya, wakazi Dodoma waalikwa kupata elimu

Imewekwa tarehe: June 24th, 2021

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kasim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya  siku ya  kimataifa ya kupambana na Dawa za kulevya ambayo kitaifa yatafanyika Mkoani Dodoma.

Katika wiki ya maadhimisho hayo shughuli mbalimbali zitafanyika katika viwanja vya Nyerere Square ikiwemo utoaji wa elimu kwa wananchi ya namna ya kuepuka dawa hizo ambazo huchangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya watu wengi hususani vijana ambao ndio nguvu kazi ya Taifa.

Akizungumza na  Waandishi wa Habari leo, Mkuu wa Mkoa Antony Mtaka amesema ni muhimu wakazi wa Dodoma wakatumia fursa hiyo kujitokeza kupata elimu ili kuepuka kujiingiza kwenye matumizi ya dawa hizo.

‘’Wakazi wa Dodoma wanakaribishwa kushiriki kupata elimu, lakini pia ni fursa kwa vijana kujitokeza kupata elimu kwani wengi wamekatisha ndoto zao kutokana na matumizi ya dawa za kulevya, watakuwepo pia wahanga wa matumizi ya dawa na wataeleza yale waliyoyapitia katika safari yao’’ amesema Mtaka.

Wakati huo huo, Mtaka amewaomba Waandishi wa Habari kutumia taaluma zao kuelimisha jamii kuhusu wiki ya maadhimisho ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ikiwemo madhara yake.

‘’nawaomba muweke uzito wa jambo hili ili tuwe na Dodoma salama hayo yakose nafasi, tutashirikiana na Mamlaka ya kudhibiti na Kupambana na Dawa za kulevya kuondoa tatizo hilo’’ amefafanua zaidi Mtaka.

Kwa upande wa Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Gellard Kusaya amesema dawa za kulevya zisipodhibitiwa nguvu kazi ya Taifa itapotea hasa vijana .

‘’Dawa hizi zinamadhara ndiyo maana zinadhibitiwa, tusipodhibiti tutakosa nguvu kazi kwa vijana, tunataka kuwa na Tanzania huru isiyotumia dawa za kulevya’’ amesema Kusaya.

Katika udhibiti wa Dawa za kulevya Kusaya amesema udhibiti umekuwa mkubwa kwani tangu ameingia madarakani kwa  mara ya kwanza wamekamata kiasi kikubwa cha dawa za kulevya kilo 859.36.

‘’hali inaonesha udhibiti wetu umekuwa mkubwa, kwa mara ya kwanza tangu Tanzania kupata uhuru tumekamata kiasi kikubwa cha dawa hizo ilikuwa ni mwezi wa nne, ni kiwango kikubwa sana cha dawa kukamatwa kwa mara moja’’, amesema Kusaya

Maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Kupambana na Dawa za  kulevya huadhimishwa June 26 ya kila mwaka, kwa mwaka huu yanakwenda sambamba na kauli mbiu isemayo ‘’Tuelimishane juu ya tatizo la Dawa za kulevya, Kuokoa Maisha’’

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.