• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri wa Afya akabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi Milioni 45

Imewekwa tarehe: May 5th, 2023

WAZIRI wa Afya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ummy Mwalimu akabidhi vifaa tiba vya Afya vyenye thamani ya shilingi Milioni 45 mkoani Dodoma vifaa vilivyotolewa  kupitia mradi wa kuboresha huduma Jumuishi za Kifua kikuu, Malaria na UKIMWI kwa Wajawazito kabla na baada ya kujifungua.

Zoezi la ugawaji wa Vifaa Tiba vya Afya lilifanyika katika kituo cha afya cha Makole kuwakilisha vituo vingine 19 ambavyo vinashiriki katika mradi huu.

Mwalimu alisema kuwa vipimo hivyo ni muhimu kwa wajawazito ili kuweza kuepusha kifafa cha mimba na vifo kwa wajawazito

“Niwapongeze  Chuo Kikuu cha Dodoma kwa kushirikiana na Liverpool School of Tropical Medicine chini ya ufadhili wa Global Fund na Takeda Pharamaceuticals kwa vifaa hivi. Najua mama wajawazito mpo hapa niwaombe mkifika kwenye Kliniki za Uzazi, Mama na Mtoto mhakikishe mnapimwa wingi wa damu, mkojo kuangalia wingi wa protini, shinikizo la damu pamoja na kusikilizwa mapigo ya moyo ya mtoto bila kutoa gharama zozote vifaa vipo, Serikali ya awamu ya sita imehakikisha upatikanaji wa dawa za kuzuia kutoka damu wakati wa kujifungua, dawa za kuongeza damu na dawa za kuzuia kifafa cha mimba katika vituo vya afya vya umma nchini’’.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma Prof. Lughano Kusiluka, alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jinsi anavyotoa kipaumbele kwenye masuala ya Afya.

"Napenda kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya katika kuimarisha huduma za Afya katika nchi yetu na hasa katika eneo hili la mama na mtoto. Katika miaka miwili ya utekelezaji wa mradi huu inaoneshwa kwamba mradi umepokelewa vizuri na matokeo yake yameanza kuonekana kwenye kiwango cha ubora". Prof Kusiluka

Aidha, Mtafiti Mkuu wa Mradi Dkt. Leonard Katalambula alieleza kua wanakusudia kuongeza idadi ya vituo vya afya, kuongeza idadi ya mikoa, kuongeza idadi ya vifaa tiba kwa vituo vitakavyo kuwa katika mradi na vilevile kuwa na kituo cha pamoja cha mafunzo kwa vitendo kwa watumishi walioko kazini.

Mradi wa kuboresha huduma jumuishi za TB,UKIMWI na Malaria ni mradi wa miaka miwili unaofadhiliwa na mfuko wa Global Fund na Liverpool School of Tropical Medicine kwa kutoa mafunzo kwa watoa hudumaza afya ya mama kabla,wakati na baada ya kujifunguaili kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.