• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wete, Dodoma Jiji kukuza ushirikiano

Imewekwa tarehe: June 22nd, 2022

Na. Shaban Ally na Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imefungua ukurasa wa ushirikiano na Baraza la Mji wa Wete kutoka Mkoa wa Kaskazini Pemba ili kuchochea maendeleo ya wananchi wa pande mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Emmanuel Chibago alipokuwa akiwakaribisha Madiwani kutoka Baraza la Mji wa Wete, Pemba waliofanya ziara ya kikazi ya siku mbili kutembelea jiji hilo.

Chibago aliwakaribisha na kusema kuwa watapata fursa ya kutembelea miradi ya maendeleo iliyopo katika Halmashauri yake. Aliwaomba wageni hao kuanzisha uhusiano wenye lengo la kuchochea maendeleo katika maeneo yao pamoja na kudumisha umoja na mshikamano. "Niwaombe ndugu madiwani wenzangu kutoka Wete kwa pamoja tuanzishe ukurasa mpya wa uhusiano kwa lengo la kuchochea maendeleo ya wananchi wetu" alisema Chibago.

Naibu Meya aliwashukuru wageni hao kwa uamuzi wao wa kulitembelea Jiji la Dodoma na kuuita kuwa ni uamuzi sahihi. “Leo nimepata furaha baada ya kuona nimepata ugeni wa madiwani kutoka Wete, wenye lengo la kutaka kujifunza kwa kile kilichofanyika. Hivyo, basi tunashukuru kwa ujio wenu na mjisikie mko nyumbani" alisema Chibago.

Kwa upande wake Mchumi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Francis Kaunda alisema kuwa jiji hilo limeweka nguvu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa lengo la kukusanya mapato kwa wingi kupitia miradi hiyo. “Kupitia kitega uchumi chetu cha hoteli tunategemea kwa mwaka kuingiza kiasi cha shilingi bilioni 1.3" alisema Kaunda.

Kaunda alisema kuwa halmashauri hiyo imefanikiwa kufikia malengo yake kwa kufanya kazi kwa kushirikiana. “Ushirikiano mzuri baina ya viongozi wa halmashauri na wataalam ndiyo msingi wa mafanikio haya tunayoyapata. Nichukue nafasi hii kuwashauri waheshimiwa madiwani kuwa mnapopanga mikakati ya kuleta maendeleo ni vizuri mkazingatia Ilani ya uchaguzi ya chama na kushirikisha wataalam wa maendeleo katika maeneo yenu” alisema Kaunda.

Nae Katibu wa madiwani wa Baraza la Mji wa Wete, Hamadi Ali alieleza kuwa amejifunza kupitia miradi ya maendeleo iliyofanyika katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na wao kama viongozi watachukua hatua za utekelezaji watakaporudi katika maeneo yao. “Kiukweli ziara yetu hii ya kuja hapa Dodoma imetufundisha ni kwa kiasi gani tunaweza kubuni njia mpya za kuongeza mapato Katika Halmashauri zetu. Hivyo, na sisi tukirudi Pemba tutakaa chini na Baraza la Madiwani kuweza kutafuta njia mpya za kuongeza mapato” alisema Ali.

Kwa upande mwingine, Diwani wa kuteuliwa wa Wete, Aisha Hamadi alitoa wito kwa viongozi wenzake wa halmashauri nyingine kutembelea Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ajili ya kujifunza juu ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao. “Wito wangu kwa viongozi wenzangu ni kwamba waje kujifunza vitu mbalimbali vya kimaendeleo kwa kuwa kuna miradi mikubwa ya maendeleo imefanyika kama vile mradi wa soko la wazi la Machinga” alisema Aisha.

Diwani huyo alitoa pongezi zake za dhati kwa madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa jitihada zao za kuifanya Dodoma kuwa na hadhi ya juu inayostahili.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.