• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wilaya ya Dodoma yazindua Chanjo ya Korona

Imewekwa tarehe: August 4th, 2021

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WILAYA ya Dodoma imemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mapenzi yake kwa watanzania kuruhusu chanjo ya UVIKO-19 kupokelewa nchini na kuongoza zoezi la uchanjaji ili kujikinga.

Shukrani hizo zilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alipokuwa akiongea na wataalam wa afya na watu waliojitokeza kuchanjwa katika uzinduzi wa chanjo ya UVIKO-19 Wilaya ya Dodoma, tukio lililofanyika katika Kituo cha Afya Makole jijini Dodoma.

Shekimweri alisema “nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kutujalia afya njema. Pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa nia yake njema na mapenzi kwa nchi yake alipokubali kupokea dozi 1,000,000 za chanjo ya UVIKO-19”.

Akiongelea usalama wa chanjo hiyo, alisema kuwa chanjo ni salama. Mheshimiwa Rais amechanja tayari. “Napenda kuwatoa hofu wale wote wenye hofu, mimi mwenyewe nimechanja jana, na leo nipo salama na kazi iendelee. Tutafute taarifa sahihi toka kwa wataalam wa afya siyo kwenye mitandao ya kijamii inayopotosha baadhi ya taarifa” alisema Shekimweri.

Kuhusu mwitikio wa watu kujitokeza kuchanja, alisema kuwa mwitikio ni mkubwa. “Jana watu waliojitokeza kuchanja ni 1,135 kwa Wilaya ya Dodoma wakati makadilio ilikuwa kuchanja watu 600. Kwa kituo cha Afya Makole jana walijitokeza kuchanja watu 194 kati ya makadilio ya kuchanja watu 200” alisema Shekimweri.

Akimkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Dodoma kuzindua zoezi la uchanjaji chanjo ya UVIKO-19, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alisema kuwa Wilaya ya Dodoma ina jumla ya vituo saba. Kituo cha Afya Makole kimejipanga kutoa chanjo ya UVIKO-19 na kimetenga maeneo mawili ya kutolea chanjo hiyo. Alisema kuwa maeneo yataongezwa kutegemea na wingi wa watu wanakavyojitokeza kuchanjwa.

Akiongelea usalama wa chanjo hiyo, Mganga mkuu huyo alisema kuwa chanjo hiyo ni salama. “Nichukue nafasi hii kuwatoa hofu wananchi. Chanjo hii ni salama na chanjo ni kinga. Tutumie nafasi hii kuhakikisha tunachanja” alisema Dkt. Method.

Nae Afisa Habari wa timu ya Dodoma Jiji FC, Moses Mpunga aliyekuwa mtu wa pili kuchanja baada ya uzinduzi huo, alisema kuwa chanjo hiyo ni muhimu. “Kwanza naipenda afya yangu, lakini pia napenda kuwalinda walionizunguka. Mimi nikichanjwa nitakuwa nipo mbali zaidi ya kupata virusi vya UVIKO-19 kwa sababu mwili utakuwa unakinga. Na hata nikipata madhara yake hayatakuwa makubwa” alisema Mpunga.

Aliwataka wakazi wa Wilaya ya Dodoma kuachana na Habari potofu dhidi ya chanjo hiyo. “Rai yangu kwa wanadodoma wanatakiwa kuachana na hadithi za kufikirika sababu maisha ni ya mtu binafsi. Asilimia kubwa ya watu wanaoshawishi wengine wasichanje wameshachanjwa” alisema Mpunga.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.