• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wito kwa wananchi kutembelea maonesho Nanenane Dodoma

Imewekwa tarehe: August 2nd, 2022

Na. Sifa Stanley, DODOMA

AFISA kilimo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Agness Woisso ametoa wito kwa wananchi kutembelea maonesho ya wakulima na wafugaji Nanenane ili wajifunze mbinu za kisasa za kilimo.

Wito huo aliutoa katika viwanja vya Nanenane, Nzuguni alipokuwa akitoa maelezo ya namna halmashauri ilivyojipanga kuhakikisha kuwa wakulima na wananchi wananufaika na maonesho hayo, tofauti na miaka iliyopita.

“Tunawakaribisha wakulima waje kwasababu teknolojia iliyopo ni nzuri na ya kisasa. Pia kuna wakulima ambao watakuwa wanatoa maelezo na elimu kwa wakulima wengine kwasababu kuna wakulima wakipewa maelezo na afisa kilimo wanakuwa kama vile hawaamini, lakini wakielekezwa na mkulima mwenzao ni vizuri zaidi, kwa hiyo kuna wakulima tumewaalika ili watoe ushuhuda” alisema Woisso.

Aidha, aliwashauri wananchi kuanzisha kilimo cha bustani nyumbani kwa kutumia teknolojia ya kisasa, ambayo itawasaidia kulima mbogamboga nyingi katika eneo dogo. Alisema kuwa teknolojia hiyo itawasaidia kujikwamua kiuchumi.

“Katika banda letu tumeandaa teknolojia mbalimbali za kilimo kwaajili ya kuwafundisha wakulima. Kuna kilimo cha bustani za mbogamboga zimelimwa katika vipando vyetu. Bustani za nyumbani kama tunavyojua jiji letu limepimwa na maeneo ya kilimo yamepungua, tunawahamasisha wakulima walime bustani za nyumbani kwa kutumia viroba ili waweze kujikwamua kiuchumi” alisema Woisso.

Akieleza namna alivyonufaika na maonesho hayo Emmi Alex, mkazi wa Meriwa alisema kuwa maonesho hayo yamempa fursa yakujifunza masuala mbalimbali ya kilimo ambayo ni muhimu kwa wananchi wote kujifunza na si wakulima peke yao.

“Nimefurahi kufika katika maonesho haya ya Nanenane kwasababu nimeona mambo mengi mazuri. Pia nimejifunza mambo ambayo sio wakulima pekee wanapaswa kujifunza hata mtu binafsi anaweza kujifunza kama vile kilimo cha bustani mtu akanufaika na kilimo” alieleza Alex.

Maonesho ya Nanenane yalianza Agosti 1, 2022 na yanatarajiwa kuhitimishwa Agosti 8, 2022 yakiongozwa na kaulimbiu isemayo “Wekeza katika kilimo, mifugo na uvuvi kwa maendeleo ya Viwanda”.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.