• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wito watolewa kwa wananchi kuweka mazingira safi

Imewekwa tarehe: August 24th, 2019

Dodoma sasa ni jiji na maeneo mengi yamepimwa, na kazi ya upimaji na upangaji mji inaendelea. Kwa hiyo hatuna budi kuhakikisha maeneo ya jiji sasa yanakuwa safi.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu wa Jiji la Dodoma Dickson Kimaro aliposhiriki katika kufanya usafi wa kila jumamosi leo kwenye eneo la kihistoria inaposemekana kuwa tembo alizama, na hapo ndipo penye asili ya jina Dodoma lililotokana na neno 'Idodomya' (alizama).

Moja na sifa ya maeneo ambayo yamepimwa ni maeneo hayo kuonekana ni masafi, na kwa hivi sasa taka zote zinatakiwa kukusanywa na kusafirishwa kwenda kwenye dampo moja tu la kisasa lililopo Chidaya.

Ikumbukwe Mkuu wetu wa mkoa alishatoa tamko akihitaji mkoa anaouongoza uwe safi. Tamko hili alilitoa Chigongwe na Jiji la Dodoma limekuwa tukiendelea kulifanyia kazi tamko hilo kwa kila jumamosi kufanya usafi wa mazingira.

Lengo ni kuwafanya wananchi wabadilike tabia, wawe na tabia ya kufanya usafi bila shuruti, wafanye usafi kwa hiari yao bila ulazima wa matangazo kutoka Jiji, polisi jamii, mgambo, au watendaji wa kata na mitaa. Kila mmoja  kwenye eneo lake la biashara au kwenye makazi.

Kimaro alikumbusha kauli mbiu ya usafi ni USAFI WA MAZINGIRA MITA TANO kuzunguka maeneo yako. Madhumuni ni kufanya maeneo ya Jiji kwa ujumla wake yawe safi wakati wote.

"Tunahitaji jiji la Dodoma kuwa la mfano kwenye maeneo yote kama tulivyo mfano mzuri kwenye makusanyo ya fedha za vyanzo vya ndani vya mapato yetu. Tunahitaji maeneo yote ya Chigongwe, Nala, Veyula hadi katikati ya Jiji kuwe safi. Hilo linawezekana kama kila mmoja akitimiza wajibu wake, shime viongozi wa kata, mitaa na wananchi tuendelee kulisimamia jambo hili", amesema Kimaro.

Hata hivyo, Kimaro alisisitiza kuwa Jiji litaendelea kufuatilia na kama mtu atavunja sheria basi atachukulia hatua za kisheria ikiwemo kupigwa faini kati ya shilingi hamsini elfu hadi shilingi laki tatu.

Kimaro alikumbusha kuwa Makamu wa Rais mama Samia alizindua kampeni ya "Dodoma ya Kijani". Na kwamba Jiji kwa kushirikiana na TFS wanatarajia kuotesha miche ya miti milioni mbili ili kudhibiti uharibifu wa mazingira unaoendelea. Miche hiyo itasambazwa kwenye maeneo mbalimbali ili watu wapande miti. "...licha ya kupanda mti, tunategemea utakapoupanda mti, uweze pia kutekeleza jukumu la kuutunza ili ukue vizuri" alisisitiza.

Mkuu huyo wa Idara ya Mazingira na Udhibiti wa taka ngumu alisema "Jambo lingine, miti iliopo na ile tutakayoendelea kuipanda tuhakikishe hatuikati hovyo. Hivi sasa kwa taratibu ambazo jiji limeweka ni kwamba hata kama mti umeupanda wewe mwenyewe, bado huruhusiwi kuukata bila kibali kutoka Jiji la Dodoma".

Akifafanua zaidi Kimaro alisema, Jiji la Dodoma limeweka sharti kwenye vibali vya ujenzi kuwa ni lazima kupanda miti isiyopungua mitano katika eneo lako la ujenzi. Miti hiyo itajumuisha miti ya kivuli na miti ya matunda. Kimaro ametoa wito kwa wananchi wa Dodoma kutokata miti na kuwazuia wote watakaobainika kutaka kukata miti.

Aidha, amekemea watu wanaotumia mifuko la plastiki myeupe ambayo ilikuwa ikitumika kama vifungashio lakini watu wamegeuza matumisi yake na kuifanya kuwa vibebeo. Amesema Waziri mwenye dhamana na Mazingira Mhe. Simbachawene ametoa muda wa wiki mbili tu wenye mifuko waisalimishe na taratibu za kuiangamiza zitafanywa na Jiji.

Mkuu wa Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu Dickson Kimaro akiongea na wananchi mara baadha ya kukamilisha zoezi la usafi wa Jumamosi katika kata ya Kikuyu Kusini mahali ambapo inasadikika tembo alizama, na ndipo penye chanzo cha jina la Dodoma (Idodomya - alizama).


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.