• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wizara yawashukia wasioendeleza viwanja, kulipa kodi

Imewekwa tarehe: November 30th, 2020

WIZARA ya ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetoa rai kwa wamiliki wote wa ardhi walio na viwanja visivyoendelezwa na kulipiwa kodi ya pango la ardhi kuhakikisha wanalipia viwanja vyao ndani ya siku kumi na nne baada ya kupokea ankara ya madai na wasipotekeleza watanyanganywa viwanja vyao na kupatiwa watu wengine.

Rai hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa Kitengo cha Kodi Wizara ya Ardhi Denis Masami wakati wa zoezi la kuhamasisha ulipaji kodi ya pango la ardhi katika mtaa wa Chidachi jijini Dodoma ikiwa ni Mkakati wa Wizara kuhakikisha wamiliki wote wa ardhi wanalipa kodi ya pango la ardhi kwa wakati.

Alisema, Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia ofisi zake za ardhi za mikoa imeanzisha utaratibu wa kuwatembelea wamiliki wa ardhi kila mwisho wa wiki kwa lengo la kuhamasisha ulipaji kodi na kutoa elimu ili kuwawezesha wamiliki wa ardhi nchini kutekeleza jukumu hilo bila shuruti.

‘’Maeneo mengi nchini yana viwanja visivyoendelezwa na wakati huo wamiliki wake hawavilipii kodi ya pango la ardhi jambo linaikosesha mapato serikali, baada ya siku kumi na nne tutaanza utaratibu wa kuzitwaa, kuvinadi ili kufidia deni na kumilikishwa kwa watu wengine’’ alisema Masami.

Mkuu huyo wa Kitengo cha Kodi Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliongeza kwa kusema, Wizara ya Ardhi inatekeleza mkakati wake wa kuhamasisha ukusanyaji kodi ya pango la ardhi kwa kushirikisha wataalamu wa sekta ya ardhi na Makamishna Wasaidizi wa ardhi katika mikoa kwa kupita nyumba kwa nyumba na kuwapelekea wadaiwa Ankara za madai ya ulipaji kodi ya pango la ardhi na maduhuli mengine yatokanayo na sekta ya ardhi ili waweze kulipa.

Akiwa eneo la Chidachi jijini Dodoma na timu yake, Masami alibaini maeneo kadhaa yasiyoendelezwa na wamiliki wake kudaiwa kodi ya pango la ardhi sambamba na ukubwa wa eneo la shule ya St Merys Dodoma kuonesha kuwa na ukubwa wa Square mita 900 wakati uhalisia ni hekta 3.5 jambo alilolieleza kuwa limeifanya shule hiyo kulipia kiasi kidogo cha kodi ya pango la ardhi.

Kwa upande wake Afisa Ardhi wa Jiji la Dodoma Ruta Rwechugura alisema, wakati wa zoezi la kuwafuatilia wadaiwa wa kodi ya pango la ardhi walibaini kukiukwa kwa baadhi ya taratibu na wamiliki wa ardhi na kutolea mfano ubadilishaji matumizi ya umiliki sambamba na baadhi ya wananchi kuuziana viwanja bila kubadilisha jina.

Aliwataka wamiliki wote wa ardhi walionunua viwanja kwenye maeneo mbalimbali nchini kuhakikisha wanabadilisha umiliki kwa kufika ofisi za ardhi katika halmashauri husika ili kuiweka ardhi yao salama na kuwasisitizia wamiliki kutobadili matumizi ya kiwanja vyao bila kufuata taratibu.

Hata hivyo, wakati wa zoezi la kuwafikia wadaiwa wa kodi ya ardhi mmoja wa wananchi aliyefikiwa na zoezi hilo Faustine Mwakalinga aliipongeza Wizara Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa uamuzi wake wa kuwafikia wamiliki wa ardhi kwa lengo la kutoa elimu na kuhamasisha ulipaji kodi ya ardhi na kuuelezea kuwa utaratibu huo unapaswa kuigwa na watendaji wengine wa  serikali katika kudai kodi kwani ni utaratibu ulio rafiki na unamhamasisha mdaiwa kulipa badala ya kuogopa.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.