• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanamichezo watakiwa kupeperusha vizuri bendera ya Jiji la Dodoma mashidano ya UMITASHUMTA

Imewekwa tarehe: May 22nd, 2023

Na. Theresia Nkwanga, Dodoma

NAIBU Waziri wa Kilimo, Anthony Mavunde ameiasa Timu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma inayoshiriki mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA), kuipeperusha vema bendera ya jiji hilo akiwasisitiza kuwa na nidhamu na maadili mema itakayowasaidia katika kufikia malengo.

Hayo aliyasema katika hafla ya ugawaji vifaa vya michezo kwa timu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma inayoshiriki mashindano ya UMITASHUMTA, iliyofanyika katika uwanja wa shule ya sekondari Dodoma.

Mavunde alisema kuwa imani yake kwa timu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni kubwa akiamini kuwa itashinda kwa kishindo. “Mimi nataka mshinde michezo yote, mkawe vinara na katika mshindi wa jumla mchukue nafasi ya kwanza. Nendeni mkaipeperushe bendera ya Jiji la Dodoma, mkacheze na kutuwakilisha vizuri, muwe mfano bora, watu wajifunze kupitia ninyi. Mmepata nafasi ya kucheza, kaonesheni vipawa na vipaji vyenu, mkawe na nidhamu na maadili, muwafanye watu wawasimulie kwa mazuri, naamini mnauwezo wa kufanya vizuri sana” alisema Mavunde.

Akiwashukuru wadau waliojitolea kuhakikisha timu ya Jiji la Dodoma inakaa kambi na kuwa na vifaa bora na toshelevu vya michezo. “Nawashukuru kwa niaba ya wanamichezo wetu wadau wote mliojitokeza, Chuo Kikuu cha Dodoma, Benki ya Zanzibar na Kampuni ya NICAS kwa michango waliyoitoa kufanikisha ninyi kukaa kambini na kupata vifaa vya michezo vyenye thamani ya shilingi 3,000,000. Siku zote huwa nafanya kwa wanafunzi wa sekondari lakini safari hii mmeniwahi mapema nimewakumbuka na wanafunzi wa shule ya msingi. Hivyo basi, namimi pia nimewaletea zawadi zangu kwaajili ya kujiandaa na mashindano” alisema Mavunde.

Naibu Waziri huyo aliwataka walimu na walezi waliochaguliwa kukaa kambini na wanafunzi wanaoliwakilisha Jiji la Dodoma katika mashindano hayo kuwalea vizuri wanamichezo hao. Alisema kuwa malezi bora kwa wanamichezo ni chachu ya ushindi ili waweze kufanya vizuri na kuipeperusha vema bendera ya Jiji la Dodoma.

Naye Afisa Elimu ya Awali na Msingi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Prisca Myalla alimshukuru Naibu Waziri kwa niaba ya wanafunzi na walimu kwa kuwakabidhi vifaa vya michezo. “Kwa niaba ya wanamichezo wote, wanafunzi pamoja na walimu, nichukue nafasi hii kukushukuru Naibu Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Anthony Mavunde, Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini kwa kutukabidhi vifaa vya michezo. Vifaa hivi vitakuwa chachu katika kuwafanya wanamichezo wafanye vizuri zaidi, hatutakuangusha, tunakuahidi tutachukua vikombe vyote katika mashindano ya UMITASHUMTA” alisema Mwl. Myalla.

Aliongezea kwa kusema kuwa timu ya Dodoma Jiji imejiandaa vizuri kushiriki mashindano ya UMITASHUMTA katika fani zote za michezo kuanzia ngoma, mpira wa miguu na michezo mingine. “Mwaka jana ngazi ya Taifa timu ya mpira wa miguu kutoka Mkoa wa Dodoma zaidi ya wachezaji robo tatu walitoka Jiji la Dodoma, kama mwaka jana tulitoa robo tatu ya wanamichezo wa mpira wa miguu, mwaka huu tunaimani wachezaji wa timu nzima ya mkoa watatoka wilayani kwetu. Tumechagua wachezaji wazuri sana kutoka katika shule mbalimbali na tumejipanga kufanya mazoezi ya kutosha” alisema Mwl. Myalla.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.