• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Zahanati ya Mpamaa yaboresha huduma Kata ya Miyuji

Imewekwa tarehe: April 18th, 2025

Na. Abdul Juma, MIYUJI

Wananchi wa Mtaa wa Mpamaa, Kata ya Miyuji jijini Dodoma, wameeleza kufurahia kwao maboresho makubwa yaliyofanywa na serikali katika Zahanati ya Mpamaa kuanzia ujenzi wa miundombinu, ununuzi wa vifaa tiba na usimikaji wa mfumo wa Tehama yamerahisisha upatikanaji wa huduma na kuboresha mazingira ya kufanyika kazi.

Katika mahojiano na wanahabari waliotembelea zahanati hiyo kwa ajili ya kufuatilia maboresho yaliyofanywa katika zahanati hiyo wananchi walielezea kufurahia maboresho hayo na huduma zinazotolewa.

Mkazi wa Mtaa wa Mpamaa, Anifa Sagika alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kuwajengea zahanati ya Mpamaa. “Hapo awali, tulikosa huduma muhimu, hasa sisi akina mama wajawazito tulilazimika kutembea umbali mrefu au kujifungulia nyumbani. Sasa tuna huduma inatolewa karibu nasi” alisema Sagika.

Nae Malimi Charles alisema kuwa anapongeza juhudi za serikali kuhakikisha huduma za afya zinapatikana katika kata hiyo. Alisema kuwa zahanati hiyo imesaidia kupunguza vifo vya wajawazito na kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya na kumtaja Rais Samia kuwa ametimiza ndoto ya muda mrefu ya wakazi wa Miyuji.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mpamaa, Happy Joshua, alieleza namna mradi huo ulivyotekelezwa kwa mafanikio. “Ninamshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza ahadi yake. Pia nawashukuru Mbunge wetu wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde, na Diwani wetu Beatrice Ngerangera kwa kushirikiana kuleta maendeleo. Zahanati hii imesaidia sana, hasa kwa huduma za mama na mtoto ambazo zamani zilifanyika chini ya mti katika kanisa la RC” alisema Joshua.

Afisa Tabibu na Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Mpamaa, Dkt. Fatuma Maseli, alisema kuwa zahanati hiyo ilipokea fedha Shilingi Milioni 43 kwa ajili ya ununuzi wa samani, vifaa tiba, pamoja na kuwekewa mfumo wa kidigitali unaorahisisha utoaji wa huduma. “Awali wagonjwa walikuwa wanakaa chini kwa kukosa viti, lakini sasa tuna mazingira bora. Pia tumepatiwa kichomea taka hatarishi na mfumo wa kisasa unaoitwa ‘Gothomis’. Tunawapongeza viongozi wetu na tunaomba Mungu azidi kuwabariki,” alisema Dkt. Maseli.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.