• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Chang'ombe yapata Kituo cha Afya, watu elfu 25 kufaidika

Imewekwa tarehe: May 27th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KITUO cha Afya Chang’ombe kinatarajia kuhudumia wakazi wapatao 25,000 kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kuwapunguzia adha wananchi ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya afya.

Kauli hiyo ilitolewa na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alipokuwa akitoa taarifa fupi ya Kituo cha Afya Chang’ombe kwa Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliyoongozwa na Mkurugenzi wake, Joseph Mafuru kutembelea kituo hicho mwishoni mwa wiki.

Dkt. Method alisema kuwa Kituo cha Afya Chang’ombe kinatarajia kuhudumia wananchi 25,000 kitakapokamilika. Alisema kuwa Halmashauri ilipokea kiasi cha shilingi 250,000,000 kutoka serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa majengo mawili na kichomea taka. Alisema kuwa majengo mawili yaliyojengwa ni jengo la wagonjwa wa nje (OPD) na jengo la maabara. Kiongelea ujenzi wa kichomea taka, alisema kuwa ujenzi huo unatarajiwa kukamilika baada ya wiki moja.

Mganga mkuu huyo aliishukuru serikali kwa uamuzi huo wa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya. Alisema kuwa eneo lote la Kata ya Chang’ombe pamoja na ukubwa wake halikuwa na kituo cha afya cha serikali.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru alisema kuwa ujenzi wa kituo hicho cha afya ni hatua nzuri kwa maboresho ya huduma za afya wananchi wa Kata ya Chang’ombe. “Kata ya Chang’ombe ina wananchi wengi. Hivyo, ujenzi wa kituo cha Afya ni uamuzi wa kimkakati katika kusogeza karibu huduma za afya kwa wananchi” alisema Mkurugenzi Mafuru.

Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilifanya ziara ya kazi kutembelea vituo vya afya vya Chang’ombe, Kizota na Nkuhungu kuona hali halisi ya utekelezaji wa ujenzi unaoendelea.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.