• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Ziara ya DC Maganga Chahwa yachanua

Imewekwa tarehe: September 12th, 2020
  • Waliojimilikisha maeneo ya umma kutimuliwa

MKUU wa Wilaya ya Dodoma Mjini Josephat Maganga leo ameendelea na ziara yake ya kujitambulisha kwa wananchi wa Wilaya anayoiongoza kwa kutembelea Kata ya Chahwa ambayo ni miongoni mwa Kata 41 zinazounda Jijini la Dodoma.

Akiongea na wananchi hao Mheshimiwa Maganga amesema "Pamoja na kujitambulisha, nimekuja pia kuangalia miradi ya wananchi ambayo inaendelea hapa Chahwa na tatu kuongea na wananchi kwa maana ya wananchi kutoa kero zao ili zishughulikiwe"

Akifafanua zaidi Mhe. Maganga aliwaomba wananchi waliojitokeza waweze kuongea ili aweze kufahamu maendeleo yao na kusikia kero ama mambo ambayo si mazuri na yanayohitaji kuondolewa.

"..tena mna bahati kubwa sana, mko karibu na ukuta wa Ikulu hapa na mnafahamu nani yuko huko Mhe. John Pombe Magufuli, siku zote ametuelekeza sisi wasaidizi wake tuwe karibu na wananchi wetu, tujue kero zao" alisisitiza Mhe. Maganga akiwapa tumaini wananchi hao.

Naye Alfa Malogo mwananchi wa Chahwa akichangia katika mkutano huo wa hadhara akatoa kero inayohusu maeneo ya wazi. "Mhemishimiwa Mkuu wa Wilaya hapa tumegawanyika makundi mawili, kuna watu ambao hawana ardhi lakini wanapotosha watu, ujue kuwa hawa wapimaji (wa Jiji la Dodoma) wanaongea ukweli.

Kuna maeneo ya wazi hapa Chahwa tunayajua, ... hawa viongozi wajumbe kuna maeneo kama saba ambayo tunayajua wamegawana hawa viongozi" alihitimisha Malogo kwa msisitizo mkubwa.

Mwananchi mwingine mwanamke ambaye hakutaja jina lake alimuomba Mkuu wa Wilaya asaidie eneo la Chahwa kupata umeme na shule ya sekondari.

"Tunaomba tupatiwe umeme ili wanawake tuweze kuutumia kufanya biashara hata za kutengeneza 'ice cream' na kujipatia kipato, pili tunaomba shule ya sekondari. Watoto wetu wamekuwa wakisoma maeneo ya mbali kama Mtumba, Msanga, Hombolo, Ipala na Mahoma, na sisi tupatiwe shule ya sekondari ya Kata" alisema mama huyo na kushangiliwa na wananchi waliojitokeza katika mkutano huo wa hadhara.

Akijibu hoja na kero zilizowasilishwa, Mhe. Mkuu wa Wilaya alitoa ufafanuzi kuwa, katika ardhi ndiyo mipango yote ya Serikali inafanyika, kama kuna uhitaji wa barabara, majosho ya kuoshea ng'ombe, reli na kadharika tunajenga kwenye ardhi.

"...ardhi pia ni uchumi, watu wanauza ardhi kupata pesa, watu ambao ardhi yao inatwaliwa kwa matumizi mengine wanalipwa pesa, ...ardhi ina mazuri, ina fujo na ina vurugu nyingi ambazo zinaweza kuepukika kama kuna mipango mizuri, lakini pia inaweza kuleta madhara kama kuna mipango mibaya" alifafanua Mhe. Maganga.

Akielezea zaidi, Mhe. Maganga alisema kuwa, kutokana na watu kuongezeka na ardhi kutoongezeka, suala la ardhi lote limewekewa sheria kwa malengo ya kutaka watu waishi vizuri na kwa amani na hakuna mtu yeyote aliye juu ya sheria.

"Maeneo yote yaliyotambuliwa kwa matumizi ya umma soko, mabwawa, mpira, chanjo zote, banio la ng'ombe, lambo la serikali na kadharika, waliojimilikisha maeneo hayo waondoke mara moja, Mkurugenzi, hii ni kazi yako toa notisi hawa watu waondoke kwenye maeneo hayo wayaache" alimalizia Mkuu huyo wa Wilaya kwa agizo la wahusika kuondoka mara moja.

Wananchi wa Kata ya Chahwa jijini Dodoma wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mhe. Josephat Maganga (hayuo pichani) wakati wa mkutano wa hadhara katani hapo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.