• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

USAID, PS3+ walidhishwa na matumizi ya GoTHOMIS Makole

Imewekwa tarehe: June 10th, 2022

KITUO cha Afya Makole kimetembelewa na Mshauri wa Mifumo ya Taarifa za Afya kutoka Shirika la Misaada la watu wa Marekani (USAID) Bi. Joy Kamunyori, aliyeambatana na Mshauri wa Mifumo ya Afya kutoka USAID-Tanzania, Makunda Kassongo, wataalam kutoka mradi wa PS3 Plus na timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Mshauri huyo alifika kituoni hapo kuona matumizi ya Mfumo Madhubuti wa Usimamizi na Uendeshaji wa Vituo vya kutolea Huduma za Afya (GOTHOMIS) na Mfumo wa Uhasibu na Utoaji wa Taarifa za Fedha kwa ngazi ya Vituo cha Kutolea Huduma (FFARS).

Matumizi ya mfumo wa GoTHOMIS yamesaidia kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato na utoaji huduma, aidha matumizi ya mfumo wa FFARS yamesaidia kuboresha usimamizi wa fedha na matumizi yake katika kituo cha Makole.

Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method, mbele ya wageni hao kwenye ziara yao kuona namna mifumo hiyo inavyosaidia katika utendaji kazi na utoaji huduma katika vituo vya afya.

Method alisema kuwa kabla ya kufunga mfumo wa GOTHOMIS, Kituo cha Afya cha Makole kilikuwa kinahudumia wateja 108,000 kwa mwaka (2017/18), kwa sasa kituo kinahudumia wateja 300,000 kwa mwaka (2021/22) ikiwa ni ongezeko la asilimia 227 sambamba na hilo kumekuwa na ongezeko kubwa la ukusanyaji wa mapato kutoka Shilingi million 84 kwa mwaka 2017/18 hadi kufikia Milioni 373 kwa mwaka wa fedha 2021/22, ikiwa ni ongezeko la asilimia 444.6 kwa kipindi cha miaka mitatu.

“Mfumo wa GOTHOMIS toleo la 4, unamuwezesha mgonjwa anapofika kituoni kusajiliwa kieletroniki na kufuatiwa na hatua zingine za matibabu kwa njia ya mfumo ikiwemo huduma za vipimo vya maabara, kuonana na daktari, kupata dawa, kulazwa na kadharika. Uwepo wa mfumo katika kituo chetu cha afya umesaidia kuongezeka kwa kasi ya utoaji huduma bora na ukusanyaji wa mapato.

Katika ukusanyaji wa mapato Kituo cha Afya Makole yameongezeka kutoka shilingi milioni 84 kwa mwaka 2017/18 hadi kufikia shilingi milioni 373 kwa mwaka wa fedha 2021/22 hilo ni ongezeko la asilimia 444.6 katika kipindi cha miaka mitatu.”

Akiongelea zaidi mafanikio ya mfumo huo, Mganga Mkuu Dkt. Andrew Method amesema kuwa mfumo umeongeza usiri wa taarifa za wagonjwa, umerahisha madaktari kuhudumia watu wengi zaidi, umesaidia upatikanaji wa taarifa mbalimbali, unaweza kutoa taarifa za utendaji kazi kwa kila mtumishi, umepunguza muda wa wagonjwa kusubiri huduma, unatoa takwimu sahihi za wagonjwa na dawa, na usimamizi wa matumisi ya dawa.

Aidha, akiongea na tovuti hii Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari, Mawasiliano na Uhusiano, Joseph Fungo alifafanua kuwa kitengo chake kinatoa msaada wa kitaalamu wa matumizi ya mifumo hiyo katika vituo vya afya 3 ambavyo tayari vimesimikwa mfumo wa GoTHOMIS ambavyo ni Makole, Mkonze na Hombolo.

“Katika kitengo changu cha TEHAMA baada ya kufunga mfumo wa GoTHOMIS katika vituo vya afya 3 kati ya 4 tulivyonavyo tuliwapatia mafunzo watumishi wote kuhusu matumizi ya mfumo huu, na ikitokea changamoto yoyote huwa tunapewa taarifa mapema na wataalamu wangu wanafika eneo husika na kushughulikia changamoto husika kwa wakati” alisema Fungo.

Hata hivyo, Afisa TEHAMA kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Baraka Samson alipokea na kuahidi kuzifanyia kazi changamoto zilizojitokeza katika mfumo huo ikiwemo kujaa mapema sehemu ya kuhifadhia taarifa za matibabu ya wagonjwa na kushuka kwa kasi ya mtandao katika baadhi ya maeneo.

“Sisi upande wa Ofisi ya Rais - TAMISEMI tumepokea changamoto hizo na tutazifanyia kazi kwa haraka ili huduma iweze kuongezeka kwa kasi na kuwa bora zaidi” alisema Samson.

Bofya hapa kuona: PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.